Mavunde agawa leseni kwa vikundi 21 Simanjiro
Simanjiro. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amekabidhi leseni kwa vikundi 21 vyenye wanachama 423 Wilaya ya Simanjiro, mkoani Manyara, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha vijana na wanawake walioko kwenye uchimbaji mdogo wa madini. Mavunde amekabidhi leseni hizo leo, Alhamisi Novemba 27, 2025, katika mji mdogo wa Mirerani wakati wa mkutano wake na wadau wa madini…