‘Kubeti’ kwatajwa chanzo kifo cha mwanafunzi UDOM
Dodoma. Wakati Jeshi la Polisi, likiendelea kuchunguza kifo cha Said Kabuga, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), aliyefariki dunia kwa kutumbukia kisimani, baadhi ya wenzake wameeleza awali alionekana mwenye mawazo akitaja fedha alizotumia kubeti. Kabuga, mwanafunzi wa mwaka wa pili chuoni hapo, pia anatajwa kwamba alikuwa mpole na mkimya, hakupenda kujichanganya na wenzake, na…