FYATU MFYATUZI: Sasa natangaza rasmi ufalme wa Fyatuland
Kuanzia sasa, Fyatuland si jamhuri tena. Ni ufalme wa Fyatu Mfyatuaji awafyatuaye mafyatu atakavyo wasifyatuke wakamfyatua. Kuwafyatua vilivyo, juzi niliwafyatua mafyatu mkenge. Walinipigia kelele wanataka domoghasia aka demokrasia. Sikusita. Kwangu, hii ilikuwa fursa ya kuwafyatua vilivyo tena bila aibu wala huruma. Niliitisha uchaguzi ambao wapinzani wangu waliuita uchafuzi. Nilishangaa. Nani alimchafua nani wakati nilichofanya ni…