Hekta 170 za Mlima Hanang zaungua moto

Hanang. Hekta 170 za hifadhi ya mazingira asili ya mlima Hanang mkoani Manyara, zimeungua moto uliodumu kwa muda wa siku tatu. Mlima Hanang una ukubwa wa hekta 5,371 na urefu wa mita 3,4200 kutoka usawa wa bahari ni wa tano kwa urefu nchini ukitanguliwa na Kilimanjaro, Meru, Loolmalasin na Oldonyo Lengai. Ofisa uhifadhi wa Wakala…

Read More

Serikali yachunguza ubadhirifu wa Sh2.5 bilioni Temesa

Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema wizara imebaini tuhuma za ubadhirifu wa Sh2.5 bilioni ndani ya Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) kufuatia uchunguzi wa awali uliofanyika baada ya kupokelewa barua ya wananchi iliyowasilishwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa vivuko Kigamboni.                                                                                                                          Ulega, amesema…

Read More

Polisi yakana kuwateka viongozi Chadema Songwe, yadai inawashikilia kwa vitendo vya uhalifu

Songwe. Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limekanusha madai ya kutekwa kwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani humo, Isakwisa Lupembe, pamoja na Meya mstaafu wa Tunduma, Ally Mwafongo, na kubainisha kuwa viongozi hao wako mikononi mwa polisi wakichunguzwa kwa tuhuma za vitendo vya kihalifu. Mvutano ulizuka baada ya taarifa kusambaa mitandaoni zikidai kuwa Lupembe na Mwafongo…

Read More

Dar City, Fox Divas watwaa ubingwa wa betPawa NBL 2025

Na Mwandishi wetu Timu ya Dar City kwa upande wa wanaume na Fox Divas kwa upande wa wanawake zimetwaa ubingwa wa mashindano ya klabu bingwa ya mpira wa kikapu Tanzania (betPawa NBL 2025) yaliyomalizika Jumamosi kwenye uwanja wa Chinangali, mkoani Dodoma. Dar City ilitwaa kombe hilo baada ya kuichakaza Kisasa Heroes kwa pointi 80-51 wakati…

Read More

Azam FC yaifumua Simba kwa Mkapa

Mechi bora ya Ligi Kuu Bara imepigwa leo kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam na Azam kumaliza ubabe wa Simba kwa kuichapa mabao 2-0. Huu ulikuwa mchezo muhimu kwa timu zote kuhakikisha zinajiweka kwenye mazingira mazuri kwenye Ligi Kuu lakini pamoja na kosakosa za kila mara bado timu zote zilishindwa kutikisa nyavu  katika…

Read More

ULEGA AMSIMAMISHA KAZI ‘BOSI’TEMESA

:::::::: SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi imemsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za uzembe, usimamizi dhaifu na ubadhirifu dhidi yake na viongozi wengine wa taasisi hiyo.  Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ametangaza hatua hiyo jijini Dar es Salaam leo akisema hatua hiyo imefuatia malalamiko ya…

Read More

Bodaboda wataka polisi imwachie diwani mstaafu Chadema

Mbeya. Vijana wa Kata ya Kiwira wilayani Rungwe wamekemea vitendo vya uvunjifu wa amani, huku wakiliomba Jeshi la Polisi kumuachia huru aliyekuwa diwani wa Kata hiyo, Simon Kiraiti (Chadema) na kumpa heshima maalumu ya mtumishi mstaafu. Wakizungumza leo Desemba 7,2025 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya udereva kwa waendesha pikipiki ‘bodaboda’ wamemshukuru Mbunge wa Mbeya…

Read More

Watumishi legelegewaonywa wilayani hai | Mwananchi

Hai. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, wametakiwa kuweka mikakati madhubuti na kutilia mkazo suala la ukusanyaji wa mapato, ili kuiwezesha halmashauri kuwaletea wananchi maendeleo yanayoonekana. Wito huo umetolewa leo, Desemba 7, 2025, na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Nzowa, katika mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika katika…

Read More