Wanafunzi 686 wakatisha masomo CUoM sababu zatajwa

Mbeya. Imeelezwa kuwa jumla ya wanafunzi 686 wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Mbeya (CUoM), wameshindwa kuhitimu masomo yao kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za vifo, utoro na kushindwa kutimiza vigezo vya kitaaluma. Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano, Desemba 17, 2025 na Kaimu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Romuald Haule, wakati wa mahafali ya 10…

Read More

Serikali yaijibu Marekani zuio kuingia nchini humo

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania, imejibu tamko la Marekani kuhusu kuweka vikwazo kwa Watanzania kutongia nchini humo. Taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatano Desemba 17, 2025 na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhusu hatua ya Marekani kuiweka Tanzania katika kundi la nchi 15 zilizowekewa udhibiti wa visa kuingia nchini…

Read More

Kocha wa Azam FC kuibukia Rayon Sports

KOCHA wa zamani wa Azam FC aliyekuwa akiinoa Wiliete Banguela ya Angola kabla ya kuondolewa hivi karibuni, Mfaransa Bruno Ferry yupo katika hatua za mwisho za kujiunga na Rayon Sports ya Rwanda, ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu alipoachana na Wiliete, Novemba 15, 2025. Kocha huyo aliachana na Wiliete, baada ya ripoti kutoka Angola kudai…

Read More

Pogba wa Zenji, Mtibwa kuna kitu!

UONGOZI wa Mtibwa Sugar upo kwenye mazungumzo na kiungo mshambuliaji wa Mlandege, Juma Kidawa ‘Pogba’ kwa ajili ya kuongeza nguvu kikosini dirisha dogo. Pogba ambaye mwanzoni mwa msimu alikuwa akihusishwa kutua Simba kabla ya mpango wake kufa baada ya wekundu hao kumnasa Daud Semfuko kutoka Coastal Union anatajwa kuwa katika hatua nzuri kuibukia Mtibwa Sugar….

Read More

JKT Tanzania yajitosa dili la Nkane

MAAFANDE wa JKT Tanzania wameingilia kati dili la kumpata kwa mkopo nyota wa Yanga, Denis Nkane, baada ya mchezaji huyo anayecheza nafasi mbalimbali uwanjani kushindwa kupenya katika kikosi cha kwanza kutokana na ushindani mkubwa uliopo. Awali, mabosi wa TRA United walikuwa wa kwanza kumuhitaji nyota huyo baada ya aliyekuwa mshambuliaji nyota wa timu hiyo, Emmanuel…

Read More

Tanzania yajibu zuio la Marekani

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imejibu uamuzi wa Marekani kuiweka nchi katika kundi la mataifa 15 yaliyowekewa uthibiti wa visa vya kuingia nchini humo, ikisema itaendelea na mazungumzo ya kidiplomasia ili kupata muafaka unaolinda maslahi ya wananchi wa pande zote. Kupitia taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iliyotolewa leo,…

Read More

Baada ya Kulandana, ni zamu ya Lyanga City

BAADA ya kumalizana na Abdallah Kulandana, uongozi wa Mbeya City uko kwenye hatua za mwisho kumalizana na aliyekuwa mshambuliaji wa Singida Black Stars, Azam FC, Ayubu Lyanga kwa ajili ya kuongeza nguvu eneo la ushambuliaji. Wakati dirisha la usajili likitarajiwa kufunguliwa mapema mwezi ujao Mbeya City tayari imeanza kusajili ikimalizana na Kulandana kwa mkataba wa…

Read More

‘Tuisaidie Serikali kujenga, kurejesha umoja’

Musoma. Askofu Mkuu wa Kanisa la Menonite Tanzania, Nelson Kisare amewaomba viongozi wa dini nchini kuisaidia Serikali kujenga na kurejesha umoja na mshikamano wa kitaifa ili kurejesha hali ya utulivu, amani na usalama nchini. Askofu Kisare ametoa wito huo mjini Musoma leo Jumatano Desemba 17, 2025 katika warsha ya elimu ya amani kwa viongozi wa…

Read More

Ushuzi wa mwanamke na siri afya ya ubongo wake

Dar es Salaam. Watafiti wamethibitisha kuwa mwanamke anapotoa upepo hapaswi kuona haya, kwani harufu kali ya ushuzi anaoutoa huenda ikawa kichocheo cha siri cha afya ya ubongo wake. Kwa wastani, binadamu hutoa ushuzi hadi mara 23 kwa siku, lakini si mara zote kila ushuzi kuwa na harufu sawa. Utafiti unaonyesha kuwa gesi ya tumbo ya…

Read More