Ahadi za Mwinyi kwa bodaboda, wakulima na wajasiriamali
Unguja. Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Hussein Mwinyi, amesema akipata ridhaa nyingine ya kuongoza, watawekeza nguvu kubwa kuyainua makundi ya wajasiriamali, huku bodaboda wakiundiwa ushirika wa kumiliki pikipiki zao wenyewe. Dk Mwinyi ametoa kauli hiyo leo, Septemba 16, 2025, wakati akizungumza na makundi ya bodaboda, wakulima wa viungo na wajasiriamali…