Mbunge adai kufanyiwa figisu asirudi bungeni

Dodoma. Homa uchaguzi mkuu wa Oktoba, 2025 imezidi kutanda ndani ya Bunge baada ya Mbunge wa Kyerwa (CCM), Innocent Bilakwate kudai kuwa kuna kiongozi anahonga pesa kwa mabalozi ili asichaguliwe. Amesema hatua ya kiongozi huyo ambaye pia ni mfanyabiashara wa kahawa imekuja baada ya Bilakwate kupambania maboresho ya bei ya kahawa. Uchaguzi mkuu wa Rais,…

Read More

ASKARI 155 WAPANDISHWA VYEO MKOANI RUVUMA

Songea-Ruvuma. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Marco G. Chilya, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura, amewapandisha vyeo askari 155 waliohitimu mafunzo ya upandishaji vyeo kwa mwaka 2024/2025 na kufaulu kwa mafanikio. Shughuli ya uvalishwaji wa vyeo hivyo imefanyika katika viwanja vya Kikosi…

Read More

Akili Mnemba ya Gemini kujumuishwa kwenye ‘Google Search’

Dar es Salaam. Ili kurahisisha utafutaji taarifa mtandaoni kampuni ya Google inayomiliki Akili Mnemba (AI) ya mazungumzo ya Gemini imeamua kuiweka programu hiyo kwenye kipengele cha kutafuta cha ‘Google Search’. Hatua hiyo inatajwa kumrahisishia mtumiaji kutafuta taarifa sambamba na kumpa uzoefu wa matumizi ya Akili Mnemba. Ikumbukwe Akili Mnemba ni teknolojia inayowezesha kompyuta na mashine…

Read More

Namna ya kuvunja mzunguko wa kuishi mshahara kwa mshahara

Kuishi kutoka mshahara hadi mshahara ni mzunguko wa kuchosha unaowatega mamilioni ya watu wanaofanya kazi kwa bidii katika hali ya sintofahamu ya kifedha. Kila mwisho wa mwezi unahisi kama kusubiri kufikia sufuri, ukisubiri mshahara mwingine ili kuendelea kuishi. Licha ya kufanya kazi kwa saa nyingi, au hata kushikilia ajira zaidi ya moja, pesa huonekana kutoweka…

Read More

Athari za ukosefu wa fedha ‘ndogo’ kwenye mzunguko

Wiki iliyopita, kulikuwa na mjadala kuhusu uwiano wa mzunguko wa fedha nchini, ambapo fedha zenye thamani kubwa manthalani noti zenye thamani ya Sh10,000 na Sh5,000 zinaonekana kuzidi zile zenye thamani ndogo kama vile Sh 500, 1,000, na 2,000. Hili ni suala ambalo limekuwa likijitokeza mara kwa mara na limejadiliwa hapa kwenye safu yetu ya Fedha…

Read More

MKURUGENZI MTENDAJI WILAYA YA MADABA AZURU HOSPITALI YA WILAYA, AWATAKA WANANCHI WAITUMIE KIKAMILIFU

Madaba_Ruvuma. Tarehe 21 Mei 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Ndugu Sajidu Idrisa Mohamed, amefanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Madaba kwa lengo la kujionea maendeleo na maboresho makubwa ya huduma za afya yanayoendelea kutekelezwa hospitalini hapo. Katika ziara hiyo, Mkurugenzi alipata fursa ya kupokea huduma ya matibabu kutoka kwa wataalamu…

Read More