Vyombo vya habari vyatakiwa kufichua rushwa uchaguzi mkuu

Dar es Salaam. Vyombo vya habari nchini vimetakiwa kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa hususani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Crispin Chalamila wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari katika warsha…

Read More

UVCCM yawaita vijana kujiandikisha kupiga kura, kugombea

Dar es Salaam. Katibu Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Jesca Mshama amewataka vijana kuchangamkia fursa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 2025. Amesema Tanzania ya sasa inahitaji viongozi vijana wenye maono mapana, weledi, uadilifu na uzalendo katika…

Read More

Fyatu afyatua figa na fwakit kuhusu Kanada

Tangu nifyatukie Kanada, nimekuwa nashuhudia mambo ya ajabu toka kwa mafyatu. Wapo wanaoomba mialiko ili waje huku wagome kurejea kwao na kufanya niwatunze hadi nifyatuke. Wapo wanaonipiga mizinga tena mingine ya kijinga siyo kifyatu. Hivi, unajisikiaje fyatu ambaye ameishastaafu kukubomu dolari 500 kwa ajili ya harusi ya kitegemezi chake na si kwa ajili ya matibabu…

Read More

Lissu mahabusu, nakumbuka nyakati za madeko za 4R

Ukweli upi unapaswa kuzungumzwa? Unaompa faraja mgonjwa lakini haumsaidii kubadili hali yake? Unaomuumiza mgonjwa, ila ndiyo ukweli wenyewe? Mimi nachagua ukweli unaoweza kuonekana ukatili. Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, yupo mahabusu. Kesi inayomkabili ni uhaini. Wakati huohuo, giza limetanda kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025. Ushiriki wa Chadema kwenye uchaguzi ni majaliwa. Inategemea busara zaidi. Swali, tumefikaje…

Read More

NIKWAMBIE MAMA: Uchaguzi ni mchezo wa makosa

Kwenye mchezo wa ndondi bondia anaweza kufanya kama aliyejisahau, akakuletea uso usiokingwa na mikono yake. Mbinu hii wenyewe wanaiita “kuuza sura.” Ukiamini kuwa kajisahau, utaingia kichwa kichwa, lakini ghafla atakuwahi na kukumaliza. Mabondia wengi wameshaumizwa kwa mtindo huu, lakini mabondia wajanja hupuuza chambo hicho na kuendelea na pambano kwa kuzingatia kanuni za mchezo. Wakati mwingine…

Read More

Chondechonde tusilirejeshe Taifa kwenye enzi ya giza

Aliposhika madaraka, Rais Samia Suluhu Hassan alionyesha siyo tu nia kwa maneno, bali pia kwa matendo kwa kuchukua hatua mbalimbali zilizolenga kuliponyesha Taifa. Rais Samia alikutana na makundi mbalimbali ya kijamii, wakiwemo viongozi wa dini, kisiasa na kimila kujadiliana juu ya mustakabali wa Taifa. Alizuia ukusanyaji wa kodi kimabavu kupitia vikosi kazi, kesi za kisiasa…

Read More

Muda unatosha mabadiliko madogo ni utashi tu wa kisiasa!

Jumamosi iliyopita tulisherehekea miaka 61 ya Muungano wetu huu adhimu na wa kipekee. Kwa hakika, Muungano wetu umeimarika, umepevuka, na umekomaa kiasi kwamba sasa tuko tayari kuchukua hatua ya pili ya kuudumisha kwa kuungana kuwa na serikali moja, nchi moja, chini ya Rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hili Rais Samia Suluhu Hassan…

Read More

DC SHAKA ATAKA WANAFUNZI KILOSA KUPATA CHAKULA SHULENI.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka, ametoa wito kwa wazazi, walimu, na watendaji wa kata kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula cha mchana shuleni. Amesisitiza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya elimu na afya kwa watoto, hivyo ni jukumu la kila mmoja katika jamii kuhakikisha suala hilo linapewa…

Read More

Sanya hatasahaulika kwa mambo haya

Unguja. Aprili 21, mwaka huu Zanzibar ilimpoteza mwanasiasa mkongwe na machachari, Muhammad Ibrahim Sanya, ambaye alifariki dunia wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Lumumba, Unguja. Sanya anatajwa kuwa machachari katika siasa za Zanzibar na alikuwa miongoni mwa wabunge waliopata fursa hiyo mapema mwanzoni mwa siasa za vyama vingi mwaka 1995. Sanya amekuwa mbunge wa…

Read More