Yanga yaifuata JKT Tanzania nusu fainali, ikiichakaza Stand United
YANGA ilichowafanyia Stand United ni kitu cha kikatili sana, baada ya kuichakaza kwa mabao 8-1, kwenye mchezo ambao iliutawala vyema, ikiwafuata JKT Tanzania katika Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho (FA). Staa wa mchezo huo uliochezwa Jumanne hii alikuwa kiungo wa Yanga, Stephane Aziz KI aliyepiga mabao manne huku Clatous Chama akifunga mawili. Beki Nickson…