Watoto watatu wafa maji kwenye lambo

Siha. Watoto tatu wa familia moja wamefariki dunia katika Kijijii cha Ngaratati, Kata ya Makiwaru wilayani Siha walipokuwa wakiogelea kwenye lambo lilijengwa na Serikali kwa ajili ya mifugo kupata maji. Diwani wa kata hiyo, Ezekiel Lukumai amewaeleza waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea Januari 2, 2025 watoto hao walipokwenda kufua nguo na kuoga. Amesema…

Read More

Sharifa, Glory Tausi warejesha fomu Bawacha

Dar es Salaam. Zikiwa zimesalia siku 13 kuelekea uchaguzi wa viongozi wa mabaraza ya Chadema, baadhi ya wagombea wameanza kurejesha fomu. Wagombea waliorudisha fomu ni Sharifa Suleiman anayewania uenyekiti wa Baraza la Wanawake Taifa (Bawacha) na Glory Tausi anayeomba kuwa naibu katibu mkuu wa Baraza hilo bara. Hatua ya wagombea hao kurejesha fomu, inatoa nafasi…

Read More

Hizi hapa shabaha mbili za Ramovic kwa TP Mazembe

Yanga itaingia rasmi kambini Avic Town leo Ijumaa kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya kuikaribisha TP Mazembe katika pambano la raundi ya nne ya Ligi ya Mabingwa kwa Kundi A, huku benchi la ufundi na vigogo wa klabu hiyo wakiweka mkakati kabambe ili kurejesha heshima anga za kimataifa. Kwa sasa Yanga ndio inayoburuza mkia katika kundi hilo,…

Read More

Wawili wafariki, 18 wajeruhiwa ajali ya ndege

California. Watu wawili wamefariki dunia huku wengine 18 wakijeruhiwa baada ya ndege ndogo aina ya Van’s RV-10 kugonga ghorofa la kitega uchumi jijini California nchini Marekani. Ajali hiyo imetokea saa 8:09 mchana wa kuamkia leo Ijumaa Januari 3, 2025 baada ya ndege hiyo isiyo ya kibiashara, yenye uwezo wa kubeba watu wanne, kugonga jengo la…

Read More

Mtoto adaiwa kujinyonga kisa kukosa nguo ya Krismasi

Mpanda. Christina Kalilo (8), mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Uruwila, wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi, anadaiwa kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia sweta, chumbani kwake. Inadaiwa chanzo cha kujinyonga ni mawazo baada ya wazazi wake kutomnunulia nguo za sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya. Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 3,…

Read More

Mwinyi amjibu Othman tuhuma za ufisadi, deni la Taifa

Unguja. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amejibu tuhuma zilizotolewa na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman kuhusu ufisadi na ongezeko la deni la taifa lisiloendana na kazi zinazofanyika. Rais Mwinyi amejibu madai hayo leo Januari 3, 2025 wakati akifungua kituo cha mabasi cha Kijangwani, akisema licha ya maendeleo yanayofanyika, wapo watu (hakuwataja) wanataka…

Read More

MOROGORO YATAJWA KANDA MAALUM UFUGAJI WA KISASA

Mkoa wa Morogoro watajwa kuwa Kanda Maalum ya ufugaji wenye tija kwa kuwa na ng’ombe wa kisasa na mashamba ya malisho kwa ajili ya mifugo. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amebainisha hayo Januari 03, 2025 katika Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro alipokuwa akizungumza na baadhi ya wafugaji wa mkoa huo akifafanua…

Read More