Afrika Kusini yatoa mshindi wa Sh30 milioni mashindano ya Quran

Unguja. Wakati yakifanyika mashindano ya kuhifadhi Quran kwa Afrika, Mohamed Amejair (23) kutoka Afrika Kusini ameibuka kidedea na kujinyakulia kitita cha Sh30 milioni, huku Rais Hussein Mwinyi akisema yanaitangaza Zanzibar kimataifa. Mashindano hayo yamefanyika leo Machi 22, 2025 katika Uwanja wa Aman Complex, Unguja mgeni rasmi akiwa Dk Mwinyi. Yamewashirikisha vijana 10 waliohifadhi Quran juzuu…

Read More

Janga shinikizo la juu la damu kwa watoto likiongezeka

Dar es Salaam. Watafiti wametahadharisha juu ya ongezeko la shinikizo la juu la damu kwa watoto wa shule za awali nchini, chanzo kikitajwa kuwa ni unene kupita kiasi. Utafiti uliofanyika katika wilaya za Kinondoni na Ilala mkoani Dar es Salaam na kuchapishwa Machi 19, 2025 katika Jarida la Italian linaloangazia magonjwa kwa watoto, unaonyesha asilimia…

Read More

Wanawake wa ADC wajitosa kusaka mwarobaini mikopo ya ‘kausha damu’

Mwanza. Wakati mikopo umiza hususan ‘kausha damu’ ikitajwa kuwa kikwazo cha wanawake kufikia malengo yao kiuchumi, Jumuiya ya Wanawake wa chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) imejitosa kusaka mwarobaini wa changamoto hiyo. Akizungumza leo Jumamosi Machi 22, 2025, walipofanya ziara katika ofisi ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Kanda ya Ziwa, Naibu Katibu Mkuu wa…

Read More

Wajawazito Mwanza kushiriki marathoni, faida zatajwa

Mwanza. Wajawazito wametakiwa kushiriki mazoezi na mbio fupi ikielezwa kwamba yanasaidia kuimarisha mwili, mzunguko wa damu na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo presha, kisukari na kupunguza uzito. Ushauri huo umetolewa Machi 21, 2025 na Mratibu wa Huduma ya Afya ya Uzazi katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Bertha Yohana, akieleza kuwa kutokana na umuhimu wa wajawazito…

Read More

Cosota ilivyokabiliana na migogoro 136 ya hakimiliki

Dodoma. Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (Cosota) imesema imepokea jumla ya migogoro 136 inayohusiana na masuala ya hakimiliki ambapo migogoro 118 imefanyiwa kazi na kumalizika, migogoro 10 imefikishwa mahakamani huku migogoro minane ikiwa kwenye hatua mbalimbali za utatuzi. Ofisi hiyo imeshiriki kutoa ushahidi kwenye migogoro 10 inayohusu hakimiliki ambayo inaendelea mahakamani mpaka sasa. Hayo yamebainishwa Ijumaa…

Read More

Dereva anayetuhumiwa kuiba mafuta, kuchoma lori akamatwa

Morogoro. Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia dereva wa lori la mafuta la kampuni ya Meru, Abubakar Mwichangwe anayetuhumiwa kula njama na kuiba mafuta aliyokuwa akisafirisha kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Lubumbashi, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kisha kuchoma moto gari hilo kwa lengo la kupoteza ushahidi. Kamanda wa Polisi Mkoa…

Read More

BALOZI NCHIMBI MSIBANI KWA HAWASSI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiwa kwenye msiba wa Bi. Damaris Simeon Hawassi, aliyekuwa mke wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Uchumi na Fedha, Dkt. Frank Haule Hawassi, nyumbani kwa marehemu, eneo la Mihuji, jijini Dodoma, leo Jumamosi, tarehe 22 Machi 2025. Mbali na kusaini…

Read More

Tanzania mbioni kuiuzia umeme kampuni ya Zambia

Dar es Salaam. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) lipo katika mchakato wa kuuza umeme kwa kampuni ya Kanona ya nchini Zambia. Tanesco imethibitisha uwepo wa mazungumzo hayo katika taarifa yake iliyotolewa leo Jumamosi Machi 22, 2025, ikisema mazungumzo hayo yalikuwa katika hatua ya awali. Meneja wa maendeleo ya biashara wa Tanesco, Magoti Mtani, amesema ni…

Read More