Profesa Janabi, wagombea wenzake kuchuana kwenye mdahalo Aprili 2
Dar es Salaam. Kama sehemu ya mchakato wa uchaguzi wa mkurugenzi mpya wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wa Kanda ya Afrika, mdahalo wa wagombea kunadi sera kwa njia ya mtandao utafanyika Aprili 2, 2025. Mdahalo huo utawahusisha wagombea kutoka mataifa manne, Tanzania ikiwakilishwa na Profesa Mohammed Janabi, mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)…