UUNGANISHAJI UMEME VIJIJINI WAFIKIA ASILIMIA 99.9

Vitongoji 33,657 vimefikiwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umesema kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Desemba 2024, vijiji vilivyounganishwa na umeme nchini vimefikia 12,301 kati ya vijiji 12,318 ambayo ni sawa na asilimia 99.9. Hayo yamebainishwa leo tarehe 5 Januari, 2025 na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mha. Jones Olotu wakati akiwasilisha taarifa ya hali ya…

Read More

Mashuhuda wasimulia Mutajura ‘alivyotekwa’ Dar

Dar es Salaam. Matukio ya watu kudaiwa kutekwa yameendelea kuripotiwa nchini, baada ya jana kudaiwa kutekwa kwa mkazi wa Dar es Salaam, Dastan Mutajura eneo la Buza -Sigara. Taarifa za kutekwa kwa Mutajura zilisambaa mtandaoni, zilidai lilitokea wakati akienda kazini akitokea nyumbani kwake eneo la Kitunda. Kutokana na taarifa hiyo, asubuhi ya leo Jumapili, Januari…

Read More

Mtalii afariki dunia, watano wajeruhiwa ajalini Ngorongoro

Arusha. Mtalii mmoja raia wa Israel ambaye jina lake halijafahamika (mwanamke) amefariki dunia huku wengine watano wakijeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumapili Januari 5, 2025 na Kaimu Meneja wa Uhusiano wa Umma wa NCAA, Hamis Dambaya imeeleza ajali hiyo imetokea…

Read More

Russia yaidungua ndege ya Ukraine, Blinken aikatia tamaa

Moscow. Vikosi vya Russia vimedungua ndege ya kivita ya Ukraine aina ya MiG-29, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumapili Januari 5, 2025 na Wizara ya Ulinzi ya Russia. Wizara hiyo imesema vikosi vya Ukraine, pia, vimepoteza makombora kadhaa yaliyotengenezwa katika mataifa ya magharibi ikiwemo gari ya kivita aina ya Bradley. “Mashambulizi 17 yaliyorushwa na…

Read More

Wajerumani wamjibu Musk akidaiwa kuingilia uchaguzi wao wa bunge 

Ujerumani. Wakati uchaguzi wa wabunge ukitarajiwa kufanyika nchini Ujerumani Februari 23, 2025, Serikali ya nchi hiyo imemshutumu bilionea wa Marekani, Elon Musk kwamba anajaribu kujiingiza kwenye uchaguzi huo kwa kukipigia debe chqmq kimoja wapo kati ya vinavyoshindana. Musk anadaiwa kukipigia debe chama cha siasa cha mrengo wa kulia cha Alternative for Germany AfD), hata hivyo…

Read More

Saido atoa masharti ya kutua KenGold

WAKATI mabosi wa KenGold wakipigia hesabu za kumsainisha aliyekuwa kiungo wa Yanga na Simba, Mrundi Saidi Ntibazonkiza ‘Saido’, nyota huyo ameweka masharti mapya kwa viongozi wa timu hiyo ya jijini Mbeya ili akaitumikie kwa miezi sita. Taarifa kutoka ndani ya timu hiyo, zimeliambia Mwanaspoti ‘Saido’ anahitaji pesa ya usajili Sh50 milioni na mshahara wa Sh12…

Read More

Simulizi hukumu kesi ya Sanga wa Chadema na wenzake- 1

Njombe. Haki imetendeka. Hii ndio kauli inayosikika vinywani mwa makada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), baada ya wenzao, George Sanga na wenzake wawili, kuachiwa huru kwa tuhuma za mauaji. Hii ni baada ya kukaa mahabusu siku 1,557 tangu walipokamatwa Septemba 26, 2020 kwa tuhuma za mauaji ya kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM),…

Read More