Uhamiaji yafungua Ligi Kuu Zanzibar kwa rekodi mbili

LIGI Kuu Zanzibar msimu wa 2025-2026 imeanza leo kwa kufanyika mchezo mmoja huku ikishuhudiwa Uhamiaji ikiweka rekodi mbili. Mechi hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mao A uliopo Unguja, Uhamiaji imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi. Rekodi ya kwanza Uhamiaji imeiweka kupitia mchezaji wake, Mohamed Mussa kufunga bao la kwanza la msimu akifanya…

Read More

Mtibwa Sugar yapeleka mechi zake Jamhuri Dodoma

Kufuatia Uwanja wa Manungu Complex uliopo Morogoro kutokukidhi vigezo vinavyotakiwa ili utumike kwenye michezo ya Ligi Kuu Bara, Mtibwa Sugar imeuchagua Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kwa mechi za nyumbani za Ligi Kuu Bara. Mtibwa Sugar iliyorejea Ligi Kuu Bara msimu huu, imeanza kwa kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Mashujaa ikiwa ugenini. …

Read More

Folz avunja ukimya Yanga, awajibu mashabiki

YANGA imeanza kwa kishindo Ligi Kuu kwa kushinda mabao 3-0 dhidi ya Pamba Jiji na kuwafanya mashabiki kuifurahia ushindi huo mnono licha ya kutofurahishwa na jinsi timu ilivyocheza, lakini Kocha Romain Folz amewashusha presha, huku akijifungia na mastaa na kuwawashia moto. Watetezi hao wa Ligi Kuu na Kombe la FA, ilipata ushindi huo…

Read More

Sowah aachiwa msala kwa Fountain Gate

MSHAMBULIAJI mpya wa Simba, Jonathan Sowah, leo ndiye aliyepewa jukumu la kuongoza mshambulizi ya timu hiyo katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara msimu huu dhidi ya Fountain Gate inayochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar. Hii ni mechi ya kwanza ya kimashindano kwa Sowah kubebeshwa jukumu hilo, awali alikosa mechi ya Ngao ya…

Read More

Aliyekutwa akisafirisha kokeni jela maisha

Arusha. Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ,imemuhukumu kifungo cha maisha jela, Hemed Mrisho, maarufu Horohoro baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya aina ya kokeni gramu 326.46. Hukumu hiyo ilitolewa Septemba 23, 2025 na Jaji Sedekia Kisanya aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi ya mwaka…

Read More

TEC yawapa onyo mapadri, watawa

Dar es Salaam. Kanisa Katoliki nchibni Tanzania limewapiga marufuku watawa, mapadri na waseminari kujihusisha na kampeni za uchaguzi za chama chochote cha siasa, wala kuvaa sare zao ili kulinda heshima na usafi wa kanisa hilo. Wito huo umetolewa leo Septemba 25, 2025 na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Wolfgang Pisa, wakati…

Read More

Mambo yamnyookea Simbu jeshini, sasa ni Sajinitaji

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda amempandisha cheo, Sajini Alphonse Simbu kuwa Sajinitaji (Staff Sergeant) baada ya kutwaa medali ya dhahabu katika mashindano ya dunia ya mbio za marathon ya kilomita 42 yaliyofanyika Tokyo, Japan. Simbu amepandishwa cheo leo, Alhamisi Septemba 25, 2025 katika Makao Makuu ya Jeshi Upanga, jijini Dar es…

Read More