UNMISS YAENDELEA KUTAMBUA MCHANGO WA TANZANIA KATIKA ULINZI WA AMANI SUDAN KUSINI
::::::::::: Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) umeendelea kutambua na kuthamini mchango wa askari kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoshiriki katika operesheni za ulinzi wa amani nchini humo. Katika hatua hiyo, askari wa Tanzania waliomaliza muda wao wa kuhudumu katika kikosi cha ulinzi wa amani cha UNMISS wamepongezwa kwa kazi nzuri waliyofanya ya…