Na Mwandishi Wetu
UWEKEZAJI wa fedha Sh..bilioni 280 unaofanywa na Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO ) katika vituo na njia za kusafirisha umeme, utaimarisha na kuleta utulivu wa upatikanaji wa umeme katika Jiji la Dar es Salaam.
“Dar es Salaam pekee kwa sasa inatumia megawati 750 kwa siku,mkoa wa Pwani unatumia megawati 100, matumizi yanayochangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za viwanda, hali iliyosababisha changamoto ya umeme kutokaa sawa.”
Amesema zilizowekwa katika vituo vya Gongo la Mboto na Kinyerezi zina uwezo mara tatu zaidi ikilinganishwa na transfoma zilizokuwepo awali, hatua itakayoongeza uthabiti wa umeme katika maeneo hayo.
Kuhusu kituo cha Mabibo, Waziri Ndejembi ameeleza kituo hicho ni muhimu kimkakati kwa kuwa awali jiji la Dar es Salaam lilitegemea kituo cha Ubungo kama kituo kikuu, lakini sasa Mabibo kitakuwa kitovu kikuu cha kupokea na kusambaza umeme, ikiwemo umeme kutoka Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.
Waziri Ndejembi amesema lengo kuu la Serikali ni kuhakikisha wakazi wa Dar es Salaam wanapata umeme wa uhakika, huku kituo cha Mabibo kikitarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu.