Jumuiya ya Wazazi Temeke yawekwa mguu sawa

 Na WANDISHI WETU

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi  ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM)  Wilaya ya Temeke, Hamis Slim, amewakata  viongozi  wa  mabaraza, kamati za utekelezaji za kata na matawi  za jumuiya hiyo kuvunja makundi  yaliyotokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 , 2029 na kufanyakazi kwa ushirikiano.

Ameyasema hayo  Dar es Salaam, leo katika ziara ya Kamati ya Utekelezaji ya  Jumuiya hiyo Wilaya ya Temeke katika Kata za Kiburugwa na Kibondemaji inayo lenga kuwashukuru   wanachama wa jumuiya hiyo kwa ushindi mkubwa wa  CCM na kuimarisha uhai wa jumuiya.

Slim, amesema  uchaguzi umekwisha  hivyo ni wakati muafaka wa kuvunja makundi, kusameheana, kupendana na  kuhudumia jumuiya kwa  ufanisi na weledi.

“Tunawapongeza  Jumuiya ya Wazazi mmeafanya kazi nzuri  katika uchaguzi mkuu na kuipatia  ushindi wa kishindo  CCM na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Sasa ni wakati wa kuleta maendeleo. Tuzike tofauti zetu zilizotokana na uchaguzi. Mwiba ulipoingia ndipo unapotokea,”amesema Slimu.

Pia amewataka kuishi kwa hofu ya Mungu, kuheshimu katiba ya CCM, kanuni na  viongozi na wanachama.

“Binadamu  anahamika kwa mambo matatu, Jambo la kwanza ni jinsi anavyo jifahamu mwenyewe. Jambo la pili ni namna  watu wengine wanavyo mfahamu na jambo la tatu ni nama anavyo fahamika na Mungu. Tusidharauliane kwa sababu mamlaka  hata za dunia na viongozi wake  zimetoka kwa Mungu,”amesema Slim.

Aidha  Slim,  ametumia ziara hiyo kutoa pole kwa wanachama wa jumuiya hiyo, CCM na  wananchi wote kwa ujumla kwa matukio yaliyojitokeza Oktoba 29, 2025 katika uchaguzi mkuu na kuwakumbusha umuhimu wa kutunza amani  ya taifa.

Naye Katibu wa Jumuiya ya Wazazi  Wilaya ya Temeke, Emmanuel  Itatiro,  amewataka  viongozi wa jumuiya hiyo katika ngazi za mashina, matawi na kata, kutekeleza wajibu wao kwa kufuata Katiba ya CCM na jumuiya hiyo, kanuni na miongozo.

Pia, amewahimiza kuwajibika  ipasanyo hususan kuitisha vikao vya kikatiba na kushughulikia  changamoto za  wananchi, hususa katika sekta za elimu, afya, malezi  na mazingira.

Ziara hiyo ya Kamati ya Utekelezaji ya  Jumuiya ya Wazazi   Wilaya ya Temeke, itapita katika kata zote za wilaya hiyo.