Straika mpya Simba apewa mitatu

SIMBA ipo katika mazungumzo na Mbeya City kwa ajili ya kumbeba jumla mshambuliaji, Baraka Mwangosi baada ya kuridhishwa na uwezo aliouonyesha katika michuano ya Mapinduzi Cup 2026. Mwangosi alikuwa na kikosi cha Simba visiwani Zanzibar kwa majaribio katika michuano ya Kombe la Mapinduzi inayofikia tamati leo kwa kupigwa mechi ya fainali kati ya Azam FC…

Read More

Folz afichua kilichomtoa Yanga, adai alishindwa kuvumilia

ALIYEKUWA kocha msaidizi wa Mamelodi Sundowns, Romain Folz, amezungumzia kufukuzwa kwake na Yanga, akieleza kuwa ilikuwa ‘matokeo ya mambo mengi ya kipuuzi’. Folz, ambaye pia aliwahi kuzinoa AmaZulu na Marumo Gallants za Afrika Kusini, alijiunga na Yanga Julai 2025 akiwa na lengo la kuendeleza mafanikio katika klabu hiyo na kuleta ushindani katika michuano ya kimataifa….

Read More

Baba Levo, AG wakwaa kisiki kesi ya kupinga ubunge Kigoma

Kigoma. Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa mbunge jimbo la Kigoma bado ngoma nzito, ndio maneno unaweza kuyatumia kuelezea uamuzi wa Mahakama, kukataa ombi la kusimamisha usikilizaji wa shauri hilo kwa muda usio na kikomo. Shauri hilo la uchaguzi, limefunguliwa na wapiga kura wanne wa jimbo hilo, Johary Kabourou, Loum Mwitu, Pendo Kombolela na…

Read More

Maeneo yatakayoamua urais wa Museveni, Bobi Wine

Dar es Salaam. Joto la kisiasa nchini Uganda linazidi kupanda huku maeneo haya  yanatarajiwa kuamua kati ya Rais Yoweri Museveni na Robert Ssentamu, maarufu Bobi Wine nani kuibuka na ushindi kwenye uchaguzi huo utakaofanyika Alhamisi ijayo. Kampeni za urais zilianza Septemba 29, 2025 huku za wabunge zikianza Novemba 10 na zinahitimishwa leo Jumanne, Januari 13,…

Read More

Wanaodaiwa kughushi nyaraka Bandari ya Dar kusomewa maelezo yao

Dar es Salaam. Jamhuri imepanga leo Jumanne, Januari 13, 2026 kuwasomea maelezo ya mashahidi na vielelezo, wafanyabiashara sita wanaokabiliwa na kesi ya kuwasilisha nyaraka za uongo katika Bandari ya Dar es Salaam na kujipatia zaidi ya Sh10bilioni zilizotokana na shehena ya mafuta. Hatua hiyo inatokana na upelelezi wa kesi hiyo ya uhujumu uchumi kukamilika. Washtakiwa…

Read More

Kitimtim cha usafiri wanafunzi wakirejesha shuleni

Dar es Salaam. Wakati muhula wa masomo wa mwaka 2026 ukianza rasmi leo, baadhi ya wanafunzi wamekutana na changamoto kubwa ya usafiri hususan kutoka Dar es Salaam kwenda mikoa mbalimbali. Katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli na vituo vidogo Manzese na Shekilango jana kulikuwa na abiria wengi wakihaha kusaka usafiri wengi wakiwa ni wazazi…

Read More