SIMBA SC YASHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA ESPERANCE DE TUNIS

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Simba imelazimishwa sare 2-2 na Esperance de Tunis katika mchezo wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa Afrika.

Katika mchezo huo Simba Sc ilifanikiwa kuongoza kwa mabao 2-0 kipindi cha kwanza kupitia kwa Shomari Kapombe na Yusuf Kagoma na kwenda mapumziko wa wakiwa mbele.

Kipindi cha pili Esperance de Tunis waliingia wakilisaka lango la Simba sc nakufanikiwa kupata bao la kwanza baada ya Lassane Kante kutoa basi ambayo ilimpata mpinzani na kwenda kufunga bao ambalo liliwapa matumaini na kufanikiwa kupata bao la pili.

Kwenye mchezo huo pia Esperance de Tunis walipata penati dakika ya za mwisho wa mchezo lakini penati hiyo hawakuweza kupata bao.