Msanii mkongwe wa muziki Tanzania, Mzee Hiza, mtunzi na mwimbaji wa wimbo maarufu wa “Tanzania Yetu”, amefariki dunia.
Mzee Hiza alikuwa maarufu kwa kutunga na kuimba wimbo Tanzania Yetu – Nchi ya Furaha ambao umekuwa ukielezea uzalendo na umoja wa Watanzania kwa miaka mingi.
Wimbo huo aliuandika akiwa na Bendi ya Atomic Jazz ya Tanga mwaka 1966/1967 na umechukua nafasi muhimu katika utamaduni wa muziki wa Tanzania.
Related
