Global Publishers
March 5, 2026
0 Comments
Chelsea imeonyesha ubora mkubwa baada ya kuichapa Aston Villa mabao 4-1 katika mechi ya kusisimua ya Ligi Kuu England.
Villa walianza vyema kwa kupata bao la mapema dakika ya 3 kupitia kwa Douglas Luiz, lakini Chelsea walijibu kwa nguvu na kusawazisha kupitia kwa João Pedro dakika ya 35 kabla ya mshambuliaji huyo kufunga tena dakika ya 45+6 na kuwapa uongozi kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili, Cole Palmer aliongeza bao lingine dakika ya 55 na kuhitimisha ushindi mnono wa Chelsea.
Wakati huo huo, Arsenal waliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Brighton & Hove Albion, bao pekee la mchezo likifungwa mapema dakika ya 9 na nyota wao Bukayo Saka.

Katika mchezo mwingine, mabingwa watetezi Manchester City walilazimishwa sare ya mabao 2-2 nyumbani dhidi ya Nottingham Forest. Forest walipata bao kupitia kwa Antoine Semenyo dakika ya 31, kabla ya Morgan Gibbs-White kuongeza la pili dakika ya 56.
Hata hivyo, City walijibu kupitia kwa Rodri dakika ya 62 na baadaye Elliot Anderson kusawazisha dakika ya 76 na kufanya mchezo kumalizika kwa sare ya 2-2.
Katika mchezo mwingine, West Ham United waliibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Fulham kufuatia bao la dakika ya 65 lililofungwa na Crysencio Summerville.