Global Publishers
March 10, 2026
0 Comments
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema wanafunzi watakaofaulu kwa viwango vya juu watanufaika na ufadhili wa masomo kupitia mpango wa Samia Scholarship unaotolewa na Serikali.
Dkt. Mwigulu amesema hayo wakati akizungumza na wanafunzi katika ziara yake mkoani Rukwa, ambapo pia aliwasilisha salamu maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Daktari Samia Suluhu Hassan anasema kwa wale watakaofaulu kwa kiwango cha juu wanapata ufadhili asilimia 100. Na sio ufadhili tu wa asilimia 100 peke yake, asilimia 100 na unaenda kusoma nchi yoyote duniani… hiyo inaitwa Samia Scholarship,” alisema Waziri Mkuu.
AKAGUA UJENZI WA SHULE MILUNDIKWA
Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu pia alikagua ujenzi wa shule mpya ya Elimu ya Awali na Msingi inayojengwa katika eneo la Shule ya Sekondari Milundikwa wilayani Nkasi, mkoani Rukwa.
Mradi huo unagharimu shilingi milioni 329.5 zilizotolewa kupitia Programu ya Kuboresha Ubora wa Elimu ya Awali na Msingi (BOOST).
