…..
Waziri wa Mambo ya Nchi,Mheshimiwa Patrobas Katambi (MB), amewasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kuwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Amewasilisha Taarifa ya Wizara,Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji,Zimamoto na Uokoaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA), mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(NUU).
Taarifa hizo zimewasilishwa katika Ukumbi wa Herman Stewart,Bungeni jijini Dodoma.




