TANTRADE INAONGOZA MAGEUZI YA SEKTA YA BIASHARA NCHINI KUPITIA MPANGO WA CART.IS

Dodoma, 25 Machi 2025

TanTrade inaongoza mageuzi ya sekta ya biashara nchini Tanzania kupitia Mpango wa CART.IS, unaolenga kuimarisha biashara ya kidijitali kwa urahisi na ufanisi zaidi.

Kupitia ujumuishaji wa mifumo ya taasisi mbalimbali na matumizi ya taratibu zisizohitaji karatasi, CART.IS inapunguza urasimu, inaokoa muda na gharama, na kurahisisha huduma kwa wafanyabiashara.

TanTrade ikiwa ni mdau muhimu wa mpango huu chini ya Mkurugenzi Mkuu Dkt. Latifa Mohamed Khamis, amebainisha kuwa kupitia Mpango huu, Tanzania inaongeza ushindani wake katika soko la kimataifa kwa kutoa huduma za haraka za kisasa na zenye kuaminika.