Katika ukurasa wa mtandao wa siku ya Jumanne tarehe 17 Machi, Joe Kent alitangaza kwamba amejiuzulu kama Mkurugenzi wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi cha Marekani kwa lengo la utawala wa utawala wa Donald Trump wa kujiunga na Israel katika vita dhidi ya Iran.
Kent alikiri wazi kwamba Marekani ilisukumwa kwenye vita dhidi ya Iran chini ya mashinikizo na ushawishi wa Israel. Alisema “dhamiri” yake ilikuwa imefarijika kwa kuacha wadhifa wake huo.
Ukweli kwamba marais wote wa Marekani, na hasa aliye madarakani hivi sasa Donald Trump, pamoja na wabunge wa nchi hiyo chini ya ushawishi mkubwa wa Israel ni siri iliyo wazi. Pamoja na hayo lakini Kent ameanika wazi kina cha ushawishi huo wa Israel nchini Marekani kiasi kwamba inaweza kuwashinikiza watawala wa Marekani na kuwachochea waanzishe vita dhidi ya nchi nyingine bila sababu halali na ya msingi.
Alithibitisha katika barua yake ya kujiuzulu kuwa Iran haikuwa “tishio lolote la karibuni” kwa Marekani.
Katika muda wa miezi tisa tu, Israel imewalaghai watawala wa Marekani kushiriki vita viwili dhidi ya Iran, vya kwanza vikiwa katika vya Juni 2025 na hivi vinavyoendelea sasa vilivyoanza Februari 28. Hata hivyo, wakati huu Marekani inashiriki kamilifu katika vita dhidi ya Iran ambapo imetuma meli zake mbili kubwa zaidi za kubeba ndege za kivita katika maji ya eneo na nyingine bado ziko njiani. Isitoshe, imetuma mamia ya ndege za kivita za kisasa kabisa hadi sasa zimefanya maelfu ya maelfu ambayo nchini Iran. Pia vituo vya vituo anga katika baadhi ya nchi za Ulaya na Kiarabu kushambulia Iran kwa kutumia ndege aina ya B-1, B-2 na B-52.
Matamshi ya Kent kuhusu uchokozi wa dhidi ya Iran yako wazi kiasi kwamba hayahitaji ufafanuzi wowote. Wataalamu wawili mashuhuri wa masuala ya kisiasa wa Marekani, John Mearshmeir na Stephen Walt, wamefafanua katika kitabu kuhusu ushawishi mkubwa ilionao Israel kwa wafanya-maamuzi wa Marekani.
Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel amekuwa akifanya safari za haraka mjini Washington kila mara Iran na Marekani zinapofanya juhudi za kidiplomasia kwa ajili ya kutatua matatizo yaliyopo kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran.
Netanyahu alitumia juhudi zake zote kumchochea Trump ajiondoe katika mapatano muhimu ya nyuklia ya Iran – yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Utekelezaji wa Pamoja (JCPOA) – mwaka 2018 ambao ulitiwa saini wakati wa urais wa Barrack Obama Julai 2015. Ni kwa sababu hii ndio maana akamwita Trump kuwa ‘rafiki mzuri na bora’ zaidi wa Israel.
Utumwa wa kupindukia wa Trump kwa utawala ghasibu wa Israel umewakasirisha raia na maafisa wa Marekani, akiwemo Kent mwenyewe.
Katika kipindi chake cha kwanza cha urais, Trump aliitambua Milima ya Golan inayokaliwa kwa mabavu ya Syria kama sehemu ya ardhi ya Israel na kuuhamishia kinyume cha sheria za kimataifa, ubalozi wa Marekani Beitul Muqaddas yaani Jerusalem kutoka Tel Aviv.
Ukweli kwamba Israel chini ya Netanyahu imeisukuma Marekani kwenye vita hivi haramu na visivyo na msingi dhidi ya Iran umewashtua washirika wengine wa Magharibi wa Washington. Ni kwa msingi huo ndio maana viongozi wa Canada, Italia na Italia wamesema vita dhidi ya Iran ni dalili ya kuporomoka mfumo unaotawala dunia. Hata Fredrich Merz Kansela wa Ujerumani, ambaye amekuwa akidai kuwa siku za Jamhuri ya Kiislamu zinahesabika, sasa anataka kusisitishwa vita na kurejeshwa juhudi za kidiplomasia katika uwanja huo.
Ikiwa washirika wa Washington huko Korea Kusini na Japan hawajakosoa waziwazi vita hivi dhidi ya Iran, ni kwa sababu wanaogopa kumkasirisha Trump.
Kabla ya kuanza vita viongozi wa Ulaya walikuwa na wasiwasi mkubwa na kumuonya Trump kuhusu taathira haswa za vita hivi, taathira ambazo kwa bahati mbaya zimeanza kuonekana wazi wazi na kuathiri nchi zao moja kwa moja.
Kwa vile sasa vitazidi kupanuka, na Iran kuendelea kulipiza kisasi dhidi ya hujuma ya maadui, ikiwa ni pamoja na kutoruhusu mafuta ya Marekani na washirika wake kupita kwenye Lango-Bahari la Hormuz, nchi za Magharibi sasa zinahisi machungu ya vita hivi kwa kupanda ghafla bei ya mafuta ambayo inaathiri uchumi wao.
Hata wito wa Trump kwa washirika wake wa Magharibi na Mashariki mwa Asia wa kuwataka watume meli za kivita ili kuweka wazi Lango la Hormuz umepuuzwa. Nchi za Ulaya zinazsema hivi “sio vita vyao”. Mkuu wa sera za kigeni wa Ulaya Kaja Kellas amesema, hivi si “vita vya Ulaya”. Waziri Mkuu wa Uingereza Starmer, ambaye nchi yake ni mshirika mkubwa zaidi wa Washington, amesema: “Uamuzi wetu unapaswa kuzingatia maslahi ya kitaifa ya Uingereza” na Uingereza “haitaingizwa katika vita hivi.”
Ukiachilia mbali Ujerumani, haswa chini ya utawala wa Fredrich Merz ambaye anaonekana kutokomaa kisiasa, viongozi wa Ulaya wana wasiwasi kwamba Trump anatumiwa vibaya kirahisi na Israel. Wamegundua kuwa Trump anatumiwa kama chombo cha kuropoka na kukariri kibubusa uongo ambao umekuwa ukienezwa na Netanyahu kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
Walimwenguni bado wanakumbuka vizuri mchoro maarufu wa katuni ulioonyeshwa na Netanyahu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambao ulidai kwamba Iran ilikuwa imebakisha wiki chache tu kabla ya kuunda silaha za nyuklia. Hata hivyo, licha ya kupita miaka mingi, mchoro huo bado haujathibitisha kivitendo madai yaliyotolewa!!!
Sasa Trump anadai mara kwa mara kwamba kama asingeshambulia vituo vya nyuklia vya Iran mnamo Juni mwaka uliopta, Tehran ingekuwa inamiliki silaha za nyuklia na kuzitumia kushambulia nchi nyingine.
Joe Kent, ambaye alikuwa mtu wa ndani wa utawala wa Trump, ameufahamisha ulimwengu ukweli huu mchungu kwamba ni Israel na lobi zake nchini Marekani ndio wameisukuma Marekani kwenye vita hivi haramu vinazidi kuwa na matokeo hatari siku baada ya nyingine. Kent pia hakuacha shaka kwa wale ambao hawakuamini kabisa kwamba Trump ni mtumwa na mtiifu kiasi hiki kwa Israel na watetezi wake.
Kwa kusalimu amri mbele ya mashinikizo ya Israel, Trump ameiletea Marekani aibu Kubwa. Israel imeisukuma Marekani kwenye vita athari zake kuwa mbaya na kubwa zaidi kuliko zile za vita vya Iraq vya mwaka 2003.