NAIBU WAZIRI MAJI ACHARUKA MKANDARASI KUTELEKEZA MRADI CHATO
………… CHATO NAIBU Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, ameagiza kukatwa fedha za mkandarasi wa kampuni ya “Peritus Exim Infrastructure Co. LTD” iliyokuwa ikitekeleza ujenzi wa mradi wa maji taka wilayani Chato mkoani Geita kutokana na kukiuka mkataba. Kwa mujibu wa mkataba huo mkandarasi alipaswa kuanza ujenzi juni 23, 2023 na kukamilisha Desemba 20, 2024….