Wafanyakazi kortini wakidaiwa kumuibia wajiri wao Sh1.478 bilioni
Dar es Salaam. Wafanyakazi tisa wa kampuni ya Vita Foam (T) Limited, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwana mashtaka ya wizi wa Sh1.478bilioni pamoja na kutakatisha kiasi hicho cha fedha, mali ya kampuni hiyo. Washtakiwa ni Herington Sakaya (29), mhasibu na mkazi wa Kigamboni; Buheri Komba (36), ofisa mauzo na mkazi wa Temeke;…