Waliorejeshwa Soko Kuu Kariakoo wahofia kuyaachia maeneo walikohamishiwa
Dar es Salaam. Zile kelele za baadhi ya wafanyabiashara kutishia kuandamana baada ya majina yao kutokuwamo kwenye orodha ya wanaotakiwa kurejea Kariakoo, sasa zimegeuka shubiri kufuatia kufunguliwa rasmi kwa soko hilo. Soko la Kariakoo lilifunguliwa Februari 8, 2026 baada ya kukarabatiwa kwa miaka minne tangu lilipoungua moto na kuteketeza mali za wafanyabiashara. Tayari baadhi yao…