Wagosi wamaliza gundu la siku 76

USHINDI wa mabao 4-1 ilioupata Coastal Union mbele ya Tanzania Prisons umeiwezesha kuondoa jinamizi la siku 76 bila ushindi Ligi Kuu Bara, huku kocha Mohammed Muya akisema haikuwa rahisi kwani bado wanaijenga timu. Wagosi wa Kaya walipata ushindi mara ya mwisho miezi miwili na siku 15 walipoinyoa Mbeya City mabao 2-0 katika mechi ya Ligi…

Read More

Mgunda alia na Yona Amos

KOCHA Mkuu wa Namungo, Juma Mgunda amesema kipigo cha bao 1-0 ilichopewa timu hiyo ugenini na Pamba Jiji kimewashtua, kwani hawakutarajia huku akimtaja kipa Yona Amos aliyechangia kuziacha pointi tatu jijini Mwanza. Namungo ilipata kipigo hicho cha tatu msimu huu katika mechi ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba na kuiacha isalie…

Read More

TEKNOLOJIA YA BRELI NI NGUZO YA MAENDELEO KWA WASIOONA

……………………. Na Carlos Claudio, Dodoma. Serikali imeahidi kuendelea kuwekeza na kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Breli pamoja na teknolojia saidizi nyingine, ili kuhakikisha watu wasioona wanapata fursa sawa za kushiriki katika maendeleo ya Taifa. Hatua hiyo inaendana na dhamira ya Serikali ya kutokumwacha mtu nyuma katika safari ya maendeleo. Kauli hiyo imetolewa leo Februari 11,2026…

Read More

Nyota Coastal aandika rekodi tatu

MABAO mawili aliyofunga mchezaji wa Coastal Union, Bakari Msimu, katika ushindi wa timu hiyo wa 4-1, dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons kwenye Ligi Kuu Bara juzi, yamemfanya nyota huyo kuandika rekodi tatu tamu muhimu kwa kikosi hicho. Nyota huyo alifunga mabao mawili juzi kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na mengine yakifungwa na Shiza…

Read More

Fikiri, Minziro wachuana Mashujaa | Mwanaspoti

MABOSI wa Mashujaa wameanza mchakato wa kutafuta kocha mpya atakayekinoa kikosi hicho cha maafande, huku makocha wawili ambao ni Fikiri Elias na Fredy Felix ‘Minziro’, anayeifundisha kwa sasa Bigman FC ya Championship wakichuana pia vikali. Hatua ya Mashujaa ya kusaka kocha huyo mpya, inajiri baada ya kuachana na Salum Mayanga, aliyeondoka baada ya kukiongoza kikosi…

Read More

Beki Dodoma Jiji arejea Uganda

ALIYEKUWA beki wa kushoto wa Dodoma Jiji, Dissan Galiwango, amesitisha mkataba wake wa miezi sita uliobakia na kikosi hicho, uliokuwa unaisha Juni 30, 2026, ambapo kwa sasa amejiunga na URA FC ya kwao Uganda kwa mkataba wa miaka miwili. Galiwango aliyejiunga na Dodoma Jiji, Agosti 16, 2024, akitokea Kagera Sugar, alisaini mkataba wa miaka miwili…

Read More

Malisa aomba tena ahirisho, kesi yake yakwama kuendelea

Moshi. Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi imeahirisha usikilizaji wa ushahidi wa upande wa mashtaka katika kesi ya jinai ya makosa ya kimtandao inayomkabili Mchungaji Godfrey Malisa, baada ya mshtakiwa huyo kuomba ahirisho akisubiri msaada wa kisheria kutoka Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS). Februari 11, 2026, mahakama hiyo ilipanga kuanza kusikiliza mashahidi wawili wa upande…

Read More

Equity kukusanya Sh200 bilioni kusaidia biashara ndogo

Dar es Salaam. Benki ya Equity imelenga kukusanya Sh200 bilioni kupitia uwekezaji wa wateja ili kuongeza uwezo wa ufadhili na kukuza utoaji wa mikopo, hususan kwa wajasiriamali wadogo na wa kati (MSMEs). Hatua hiyo itatekelezwa kupitia akaunti maalumu ya amana ya muda wa miaka mitatu iitwayo ‘Wekeza’, inayoruhusu uwekezaji kuanzia Sh500,000 na kutoa faida ya…

Read More

AFCON 2027 YACHOCHEA MAENDELEO YA KILIMO KANDA YA KASKAZINI

Na Pamela Mollel,Arusha  Maandalizi ya Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yameibua fursa mpya za kukuza sekta ya kilimo katika Kanda ya Kaskazini, huku viongozi wakihimizwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili kukidhi mahitaji yatakayoongezeka wakati wa mashindano hayo. Akifungua kikao kazi cha uhamasishaji na uendelezaji wa Shoroba za Kilimo leo Jumanne, Februari…

Read More