Huko Prisons kimenuka, Otieno anahesabiwa saa tu
‘LOLOTE linaweza kutokea’. Ni kauli ya Mtendaji Mkuu wa Tanzania Prisons, Godfrey Madegwa akielezea hatma ya kocha mkuu wa timu hiyo, Mkenya Zedekiah Otieno kutokana na matokeo yasiyoridhisha iliyonayo maafande hao wa Magereza. Habari za ndani zilizonaswa na Mwanaspoti zimedai Otieno alipewa mechi tatu ikiwa ni kipimo cha mwenendo alionao klabuni, ambapo mechi ya jana…