Kuwa makini mitandao isikuvunjia ndoa yako

Tuanze na kisa kilichotokea nchini Marekani mwaka jana. Mwanandoa mmoja alimtoa roho mwenzie kisa mitandao ya kijamii na tamaa. Wanandoa hawa waliokuwa wamedumu miaka 10 walijikuta pakanga. Baba alipokea baruapepe toka kwa matapeli ikimtaarifu kuwa atarithi dola za Kimarekani milioni 30.

Naye bila kufanya ajizi, alimtaarifu mwenzake bahati hii ya kupata fedha ambayo hakuitolea jasho wala kutegemea. Taarifa hii iligeuka mauti kwa mume. Bibi tamaa ilimuwaka akaamua kumpa sumu ili arithi yeye utajiri huu wa ghafla bin vu.

Mwanamke alianza kuota matanuzi, tena akiwa pekee asijue mwishowe utakuwa majuto, dhambi, kosa la mauaji na kifungo cha miaka 25. Baada ya kuwa amemwekea sumu mumewe, mke alianza kuwasiliana na mtu (tapeli) aliyekuwa amemtumia baruapepe mumewe. Haukupita muda akagundua kuwa kumbe ile baruapepe ilikuwa kanyabwoya. Hakuwa na la kufanya, bali kumwibia siri shoga yake akiwa mwingi wa hasira, majuto, na simanzi kwa ukatili na upumbavu wake mbali na roho mbaya, tamaa, na ukatili. Maji yalikuwa yameishamwagika.

Hapa unajifunza nini? Mosi, si kila ving’aravyo ni dhahabu. Pili, majuto ni mjukuu. Na tatu, tamaa mbele mauti nyuma. Maskini kiumbe asiye na hatia alipoteza maisha yake bila kosa.

Kisa cha pili ni cha mama tajiri aliyefiwa na mumewe na kuamua kutafuta mwenza mtandaoni. Huyu mama alipata mtarajiwa aliyetokea kumpenda. Muda haukupita, wawili walikutana na wakaamua kuishi kama mke na mume. Kama kwenye kisa cha kwanza, kabla ya kukubali kuishi pamoja, mama alimwamini mwenzie na kumwambia kuwa alikuwa amerithi dola milioni saba za Kimarekani. Jamaa alipiga konde moyo na kuingia ndoa ya mashaka.

Haukupita muda baba akaamua kumuua yule mama ili arithi pesa hii nono. Baada ya mama kuwa amezikwa, kumbe kuna kitu alikuwa amemficha ambacho ni watoto wake wawili wa kiume ambao walikuwa ndio warithi wa fedha husika.

Kutokana na namna mama alivyouawa, watoto waliamua kuajiri mpelelezi aliyefumua kila kitu na kugundua ukweli kuwa kumbe yule baba alikuwa amemuua yule mwanamke aliyemwamini. Kufupisha kisa kirefu, jamaa alihukumiwa kifungo cha maisha bila msamaha.

Mara nyingi, ndoa nyingi zimeyumba, kuimarika au kuvunjika kutokana na wanandoa wanavyotumia mitandao ya kijamii, hasa simu na baruapeppe zao. Si ajabu kusikia malalamiko kuwa wanandoa hawawezi kupokea hata kugusa simu za wenzi wao.
Mwanandoa yeyote mwenye siri zake na mambo yake yasiyofaa, hawezi kumpa nywila ya simu yake mwenzake. Hii ni kutaka kuficha mambo yake ya hovyo. Hata hivyo, kila lenye mwanzo lina mwisho. Wengi wanaofanya hujikuta wakijuta baada ya kuwakosa wale waliowahitaji.
Pamoja na kwamba haya mambo yapo, yupo mmoja aliyewashangaza hata kuwahuzunisha watoto wake. Siku moja aliingia maliwatoni kuoga. Bahati mbaya alisahau simu yake chumbani. Mara simu ikaita. Wakati ikiita, alisikia, bila kujali, alichomoka maliwatoni kuwahi simu. Mkewe hakuwa akimshuku kwa lolote. Hivyo, aliamua kuinyakua simu na kuipokea.
Mara sauti ya kike ikasikika ikisema “darling mbona unachelewa kupokea simu?” Yule mama hakufanya papara. Alimtaka mumewe apokee simu. Mume aliikata. Mama alikubali yaishe japo hayakuisha. Alikwenda kwa wataalamu wa mitandao wakamfundisha jinsi ya kuidukua ile simu. Baada ya kupata ushahidi wa kutosha, mama alichukua zile taarifa na kuzinakili kwenye simu yake. Siku isiyo jina si alimtolea baba kila kitu. Baba alijikuta kanaswa na tundu bovu kiasi cha kuadhirika na kusababisha ufa kwenye ndoa yake.

Related Posts

▪️Serikali kupunguza ada ya kodi ya pango kwa mwaka kwa Leseni ya chumvi ▪️Rais Samia apongezwa kwa kiwanda cha kusafisha chumvi Lindi ▪️Wazalishaji wa chumvi wafurahia kuanza kwa kodi ya zuio ▪️Serikali kudhibiti uingizaji wa chumvi kiholela nchini Dar es Salaam Katika kuwajengea uwezo wazalishaji wa chimvi nchini,Serikali imekuja na mikakati mbalimbali kufikia azma hiyo ikiwemo upunguzaji wa ada ya pango kwa mwaka ya leseni (Annual Rent) za uchimbaji mdogo wa chumvi nchini ili kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuchochea uzalishaji wa wingi wa chumvi nchini. Hayo yamesemwa jana tarehe 15 Julai, 2025 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga Kikao cha wadau wa sekta ndogo ya chumvi chini ya Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA). "*Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* ameendelea kutubeba sekta ya madini na wachimbaji kwa ujumla. Ni yeye aliyetuelekeza kusikilize kilio chenu na kutatua changamoto zinazowakabili ili mnufaike na shughuli mnazofanya" "Ametuelekeza Wizara ya Madini tuliridhie ombi lenu na kupunguza ada ya pango ya mwaka ya leseni ya uchimbaji mdogo kutoka Shilingi 45,000 mpaka Shilingi 20,000 kwa hekta, hili linakwenda kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora wa chumvi ya mzalishaji mdogo" alieleza Mhe. Mavunde. Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo udhibiti wa chumvi inayoingizwa kutoka nje ya nchi, zimepelekea bei ya chumvi ghafi kuongezeka na hivyo kuwanufaisha zaidi wazalishaji wadogo wa chumvi nchini. Uanzishwaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili (2%) kwenye mauzo ya chumvi ghafi kwa wazalishaji wenye leseni za PML imekuwa ni neema na manufaa kwao badala ya utaratibu wa awali wa kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato, ambao ulikuwa ni kero kubwa kwa wazalishaji wadogo. Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde alieleza kuwa Kiwanda cha kuzalisha chumvi cha STAMICO kipo hatua za mwisho, na kuagiza Shirika hilo kuhakikisha kabla ya mwezi wa Agosti kuisha kiwe kimekamilika na kuanza uzalishaji wa chumvi ili kupanua wigo wa soko la chumvi ya wazalishaji wadogo. Awali, akitoa taarifa ya utendaji wa Taasisi yao, Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Bi. Hawa Ghasia aliishukuru Serikali kwa kushughulikia changamoto zilizokuwa zinaikabili sekta ndogo ya chumvi nchini ambazo zimepelekea bei ya chumvi kupanda na kuwanufaisha zaidi wazalisha chumvi nchini.

▪️Serikali kupunguza ada ya kodi ya pango kwa mwaka kwa Leseni ya chumvi ▪️Rais Samia apongezwa kwa kiwanda cha kusafisha chumvi Lindi ▪️Wazalishaji wa chumvi wafurahia kuanza kwa kodi ya zuio ▪️Serikali kudhibiti uingizaji wa chumvi kiholela nchini Dar es Salaam Katika kuwajengea uwezo wazalishaji wa chimvi nchini,Serikali imekuja na mikakati mbalimbali kufikia azma hiyo ikiwemo upunguzaji wa ada ya pango kwa mwaka ya leseni (Annual Rent) za uchimbaji mdogo wa chumvi nchini ili kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuchochea uzalishaji wa wingi wa chumvi nchini. Hayo yamesemwa jana tarehe 15 Julai, 2025 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga Kikao cha wadau wa sekta ndogo ya chumvi chini ya Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA). "*Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* ameendelea kutubeba sekta ya madini na wachimbaji kwa ujumla. Ni yeye aliyetuelekeza kusikilize kilio chenu na kutatua changamoto zinazowakabili ili mnufaike na shughuli mnazofanya" "Ametuelekeza Wizara ya Madini tuliridhie ombi lenu na kupunguza ada ya pango ya mwaka ya leseni ya uchimbaji mdogo kutoka Shilingi 45,000 mpaka Shilingi 20,000 kwa hekta, hili linakwenda kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora wa chumvi ya mzalishaji mdogo" alieleza Mhe. Mavunde. Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo udhibiti wa chumvi inayoingizwa kutoka nje ya nchi, zimepelekea bei ya chumvi ghafi kuongezeka na hivyo kuwanufaisha zaidi wazalishaji wadogo wa chumvi nchini. Uanzishwaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili (2%) kwenye mauzo ya chumvi ghafi kwa wazalishaji wenye leseni za PML imekuwa ni neema na manufaa kwao badala ya utaratibu wa awali wa kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato, ambao ulikuwa ni kero kubwa kwa wazalishaji wadogo. Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde alieleza kuwa Kiwanda cha kuzalisha chumvi cha STAMICO kipo hatua za mwisho, na kuagiza Shirika hilo kuhakikisha kabla ya mwezi wa Agosti kuisha kiwe kimekamilika na kuanza uzalishaji wa chumvi ili kupanua wigo wa soko la chumvi ya wazalishaji wadogo. Awali, akitoa taarifa ya utendaji wa Taasisi yao, Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Bi. Hawa Ghasia aliishukuru Serikali kwa kushughulikia changamoto zilizokuwa zinaikabili sekta ndogo ya chumvi nchini ambazo zimepelekea bei ya chumvi kupanda na kuwanufaisha zaidi wazalisha chumvi nchini.