Y.H Malundo wenzake wanne wala nondo Marekani

 

MKAGUZI maarufu wa mahesabu hapa nchini, Yona Hezekiah Malundo kupitia kampuni yake ya Y.H Malundo na wenzake wanne wametunukiwa udaktari wa heshima kutoka Chuo Kikuu cha Read Impact kilichopo Colorado nchini Marekani. Anaripoti Makuburi Ally, Dar es Salaam … (endelea).

Tukio hilo la heshima lilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Tanganyika 2 ulioko kwenye hoteli ya Land Mark Ubungo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.

Kwa tukio hilo, Tanzania imepokea heshima ya aina yake kwa watanzania kwa sababu ya umahiri wa walioonesha.

Akizungumza katika hafla hiyo mwakilishi wa Chuo hicho, Askofu Dk. Peter Rashid Abubakar alisema tuzo hizo zimetokana na uwasilishaji wa CV zao kwa chuo hicho.

Dk Rashid alisema baada ya kukabidhiwa vyeti hivyo hivi karibuni watakabidhiwa vyeti vya utambulisho kutoka katika chuo hicho ili waendeleze gurudumu la maendeleo ya Taifa.

“Tuzo zilizopokelewa ni heshima kwao na Taifa kwa ujumla, kinachotakiwa ni utekelezaji wa majukumu inavyotakikana ndani na nje ya nchi,” alisema.

Dk Rashid ambaye ndiye mratibu wa chuo hicho kwa nchi tano ikiwemo Tanzania, Rwanda, Uganda na nyinginezo, aliwapongeza waliotunukiwa udaktari huo kwamba wamefanya kazi zao inavyotakiwa ambako anatumia fursa hiyo kuiasa jamii kuandaa CV zao ili waweze kutunukiwa udaktari na chuo hicho.

Chuo hicho msingi wake ni dini na kueleza kwamba udaktari huo wa heshima ni kazi zao zimeonekana katika jamii.
Alisema kwa kuwa yeye ni mhadhiri wa tawi la chuo hicho hapa nchini anatoa wito kwa vijana kujiandaa ili kifunguliwe chuo hicho hapa nchini.

Wengine waliotunukiwa vyeti vya udaktari wa heshima ni Mkurugenzi Mkuu Jenga Africa Empowering Society Build Nation (ESBN), Dk Paul Kanijo, Mkurugenzi wa Mesodate Consultants ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Millenium Solution Development Trust Fund, Dk Emmanuel Jeremiah.

Wengine ni Dk Boniface Mbelwa na mkewe Dk Chriatian Robert Mbelwa ambao ni mke na mume.

Aidha naye Diwani wa Viti Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Juliet Banigwa aliwapongeza madaktari wenzake kwa tuzo hizo za udaktari sambamba na kumshukuru Dk Rashid.

Dk Juliet alisema tuzo hizo ni furaha na heshima kubwa kwa nchi kwani wataendelea kuwainua na kuwaimarisha watu na jamii kwa ujumla.

Dk Malundo alisema udaktari aliotunukiwa atautumia kwa wasiojiweza kwa sababu ndio eneo lake kuwasaidia wenye uhitaji.
Mkurugenzi wa Jenga Africa, Dk Kanijo alimshukuru Mungu kwa sababu wamesimama muda mrefu kuitumikia jamii.

Dk Kanijo alisema tuzo hizo ni jambo jema na baraka ambako anajisikia fahari na wataongeza jitihada zaidi katika utekelezaji wa majukumu.

Dk Jeremiah alisema watatekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi ili kuimarisha ujenzi wa Taifa.

About The Author

Related Posts

▪️Serikali kupunguza ada ya kodi ya pango kwa mwaka kwa Leseni ya chumvi ▪️Rais Samia apongezwa kwa kiwanda cha kusafisha chumvi Lindi ▪️Wazalishaji wa chumvi wafurahia kuanza kwa kodi ya zuio ▪️Serikali kudhibiti uingizaji wa chumvi kiholela nchini Dar es Salaam Katika kuwajengea uwezo wazalishaji wa chimvi nchini,Serikali imekuja na mikakati mbalimbali kufikia azma hiyo ikiwemo upunguzaji wa ada ya pango kwa mwaka ya leseni (Annual Rent) za uchimbaji mdogo wa chumvi nchini ili kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuchochea uzalishaji wa wingi wa chumvi nchini. Hayo yamesemwa jana tarehe 15 Julai, 2025 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga Kikao cha wadau wa sekta ndogo ya chumvi chini ya Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA). "*Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* ameendelea kutubeba sekta ya madini na wachimbaji kwa ujumla. Ni yeye aliyetuelekeza kusikilize kilio chenu na kutatua changamoto zinazowakabili ili mnufaike na shughuli mnazofanya" "Ametuelekeza Wizara ya Madini tuliridhie ombi lenu na kupunguza ada ya pango ya mwaka ya leseni ya uchimbaji mdogo kutoka Shilingi 45,000 mpaka Shilingi 20,000 kwa hekta, hili linakwenda kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora wa chumvi ya mzalishaji mdogo" alieleza Mhe. Mavunde. Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo udhibiti wa chumvi inayoingizwa kutoka nje ya nchi, zimepelekea bei ya chumvi ghafi kuongezeka na hivyo kuwanufaisha zaidi wazalishaji wadogo wa chumvi nchini. Uanzishwaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili (2%) kwenye mauzo ya chumvi ghafi kwa wazalishaji wenye leseni za PML imekuwa ni neema na manufaa kwao badala ya utaratibu wa awali wa kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato, ambao ulikuwa ni kero kubwa kwa wazalishaji wadogo. Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde alieleza kuwa Kiwanda cha kuzalisha chumvi cha STAMICO kipo hatua za mwisho, na kuagiza Shirika hilo kuhakikisha kabla ya mwezi wa Agosti kuisha kiwe kimekamilika na kuanza uzalishaji wa chumvi ili kupanua wigo wa soko la chumvi ya wazalishaji wadogo. Awali, akitoa taarifa ya utendaji wa Taasisi yao, Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Bi. Hawa Ghasia aliishukuru Serikali kwa kushughulikia changamoto zilizokuwa zinaikabili sekta ndogo ya chumvi nchini ambazo zimepelekea bei ya chumvi kupanda na kuwanufaisha zaidi wazalisha chumvi nchini.

▪️Serikali kupunguza ada ya kodi ya pango kwa mwaka kwa Leseni ya chumvi ▪️Rais Samia apongezwa kwa kiwanda cha kusafisha chumvi Lindi ▪️Wazalishaji wa chumvi wafurahia kuanza kwa kodi ya zuio ▪️Serikali kudhibiti uingizaji wa chumvi kiholela nchini Dar es Salaam Katika kuwajengea uwezo wazalishaji wa chimvi nchini,Serikali imekuja na mikakati mbalimbali kufikia azma hiyo ikiwemo upunguzaji wa ada ya pango kwa mwaka ya leseni (Annual Rent) za uchimbaji mdogo wa chumvi nchini ili kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuchochea uzalishaji wa wingi wa chumvi nchini. Hayo yamesemwa jana tarehe 15 Julai, 2025 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga Kikao cha wadau wa sekta ndogo ya chumvi chini ya Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA). "*Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* ameendelea kutubeba sekta ya madini na wachimbaji kwa ujumla. Ni yeye aliyetuelekeza kusikilize kilio chenu na kutatua changamoto zinazowakabili ili mnufaike na shughuli mnazofanya" "Ametuelekeza Wizara ya Madini tuliridhie ombi lenu na kupunguza ada ya pango ya mwaka ya leseni ya uchimbaji mdogo kutoka Shilingi 45,000 mpaka Shilingi 20,000 kwa hekta, hili linakwenda kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora wa chumvi ya mzalishaji mdogo" alieleza Mhe. Mavunde. Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo udhibiti wa chumvi inayoingizwa kutoka nje ya nchi, zimepelekea bei ya chumvi ghafi kuongezeka na hivyo kuwanufaisha zaidi wazalishaji wadogo wa chumvi nchini. Uanzishwaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili (2%) kwenye mauzo ya chumvi ghafi kwa wazalishaji wenye leseni za PML imekuwa ni neema na manufaa kwao badala ya utaratibu wa awali wa kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato, ambao ulikuwa ni kero kubwa kwa wazalishaji wadogo. Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde alieleza kuwa Kiwanda cha kuzalisha chumvi cha STAMICO kipo hatua za mwisho, na kuagiza Shirika hilo kuhakikisha kabla ya mwezi wa Agosti kuisha kiwe kimekamilika na kuanza uzalishaji wa chumvi ili kupanua wigo wa soko la chumvi ya wazalishaji wadogo. Awali, akitoa taarifa ya utendaji wa Taasisi yao, Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Bi. Hawa Ghasia aliishukuru Serikali kwa kushughulikia changamoto zilizokuwa zinaikabili sekta ndogo ya chumvi nchini ambazo zimepelekea bei ya chumvi kupanda na kuwanufaisha zaidi wazalisha chumvi nchini.