HADITHI: Bomu Mkononi – 27


Nilipomaliza, nilitoka nikaenda kufungua friza na kuitazama hiyo nyama iliyoletwa. Nikamuita mtumishi wetu.

“Njoo na kisu na sufuria,” nikamwambia.

Mtumishi huyo alipofika nilichukua kisu nikakata pande la nyama na kulitia kwenye sufuria.

“Kaikatekate uibandike jikoni.”

“Niikaange?”

“Hapana, ichemshe kwanza.”