Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu akipokewa na viongozi na wafuasi wa chama hicho alipowasili kwenye Viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya kuzindua kampeni ya ‘No reforms, no election’ leo Jumapili, Machi 23, 2025.
Lissu amewasili kwenye viwanja hivyo akiwa ameongoza na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Wilbrod Slaa. Pia, alikuwepo Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara, John Heche ambao walipokewa na Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.