Kali Ongala siku 139 mechi tatu

KOCHA Mkuu wa KMC, Kali Ongala amepata ushindi wake wa tatu ndani ya timu hiyo katika kipindi cha siku 139 tangu akabidhiwe kikosi hicho Novemba 14, 2024 akichukua nafasi ya Abdihamid Moallin aliyetimkia Yanga.

Katika mechi hizo zote tatu alizoshinda, zimechezwa uwanja wao wa nyumbani wa KMC uliopo Mwenge, Dar es Salaam.

Ushindi wa kwanza kwa kocha huyo ulikuwa Desemba 16, 2024 wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Jiji kupitia bao la Hance Masoud dakika ya 88.

Related Posts