Yanga yashinda ikiweka rekodi rekodi tatu

MABINGWA watetezi, Yanga wameendelea kunyatia ubingwa wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Fountain Gate, katika mchezo uliopigwa Jumatatu hii kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo Babati mkoani Manyara huku ushindi huo uliofanya Yanga kufikisha pointi 70, umeweka rekodi tatu ndani ya kikosi hicho.

Rekodi ya kwanza inamuhusu mfungaji wa mabao mawili, Clement Mzize ambaye sasa amefikisha mabao 13 akiwa kinara wa ufungaji Ligi Kuu Bara kwa sasa.

Kwa kufikisha idadi hiyo ya mabao, maana yake Mzize amefunga mara mbili zaidi ya ilivyokuwa msimu uliopita ambapo alimaliza na mabao sita na asisti saba.

Related Posts