Yaliyojificha sakata la kipa Fountain Gate

Nyuma ya adhabu ya kusimamishwa kwa kipa John Noble wa Fountain Gate kuna sababu mbili kubwa ambazo zimefanya timu hiyo ambayo inatumia Uwanja wa Tanzanite Kwaraa Babati, Manyara kuchukua uamuzi huo.

Muda mfupi baada ya Fountain Gate kupoteza mchezo dhidi ya Yanga kwa mabao 4-0 juzi Jumatatu kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, uongozi wa timu hiyo uliamua kumsimamisha Noble ambaye hivi sasa amesharejea kwa Nigeria akingojea uamuzi dhidi yake.

“Ni kweli uongozi wa Fountain Gate umemsimamisha kipa John Noble kwa ajili ya kupisha uchunguzi dhidi yake. Uamuzi huo umechukuliwa kwa ajili ya usalama wa mchezaji mwenyewe maana baada ya mchezo watu wengi walionyesha kutofurahishwa naye,” alisema ofisa habari wa timu hiyo.

Related Posts