BEKI wa KMC, Raheem Shomary akiwa katika harakati za kuipambania timu hiyo ishishuke daraja ikiwa imebakiza mechi nne mkononi huenda akawa sehemu ya kikosi kitakachoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao.
Ipo hivi. Beki huyo ambaye aliibuka mchezaji bora msimu uliopita 2023/24 yupo katika hatua za mwisho kumalizana na Al Hilal ya Sudan.
Chanzo cha kuaminika kutoka kwa rafiki wa karibu wa mchezaji huyo kililiambia Mwanaspoti kuwa mazungumzo ya pande mbili kati ya mchezaji na uongozi wa Al Hilal yanakwenda vizuri na muda wowote beki huyo anaweza kusaini mkataba.
<