Junguni United yafunga mjadala wa iliyowatimua

SIKU tatu tu tangu Junguni United iliyopo Ligi Kuu ya Zanzibar kutangaza kuwafukuza wachezaji saba kwa tuhuma za kubeti na wachezaji hao kujibu mapigo kupitia kampuni ya uwakili ilitaka waombwe radhi ndani ya siku 14 na kulipwa fidia ya Sh300 milioni, klabu hiyo imesema imefunga mjadala huo.

Junguni inayoshika nafasi ya 12 katika msimamo wa ZPL ikiwa miongoni mwa timu nne zilizopanda daraja msimu huu sambamba na vinara wa ligi hiyo, Mwembe Makumbi, Telekeza na Inter Zanzibar ilisimamisha wachezaji hao kwa tuhuma za kubeti katika mechi mbili za Ligi Kuu dhidi ya Malindi na New City, lakini wachezaji wakakimbilia kwa mwanasheria kwa madai wamepakaziwa na hawakuitwa kujitetea kabla ya kupewa adhabu hizo zilizowafanya wapoteze haki kama wachezaji wa timu hiyo.

Wachezaji hao saba waliotimuliwa kwa tuhuma hizo ni; Salum Athumani ‘Chubi’, Ramadhan Ally Omar ‘Matuidi’, Abdallah Sebastian, Danford Mosses Kaswa, Bakari Athumani ‘Jomba Jomba’, Rashid Abdalla Njete na Idd Said Karongo, huku kampuni ya uwakili inayowasimamia katika shauri hilo ni The Lord Whiteman & Company Advocates ya jijini Dar es Salaam chini ya wakili Kasigwa Ayoub.

Related Posts