Chombo cha kusimamia miundombinu ya michezo kuanzishwa

Serikali imeanza mchakato wa kuanzisha chombo maalumu cha usimamizi wa miundombinu ya michezo katika kukabiliana na changamoto za uendeshaji wa miundombinu ya michezo nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi leo Mei 7, 2025 wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2025/26.

Profesa Kabudi amesema chombo hicho kitakuwa na mamlaka ya kusimamia uendeshaji, ukarabati na matunzo ya miundombinu yote ya michezo nchini.

“Hivyo, ni matumaini yetu kwamba kuwapo kwa chombo hiki kutapunguza changamoto za usimamizi wa miundombinu na kutaongeza thamani ya miundombinu ya michezo nchini,” amesema Profesa Kabudi.

Wakati Tanzania itaandaa fai

Related Posts