Puma Energy Tanzania yakabidhi zawadi shindano la uchoraji kampeni ya Usalama Barabarani Mashuleni

Hii inadhihirisha dhamira ya Puma Energy Tanzania ya kujenga mustakabali salama kupitia sera yetu ya Afya, Usalama, na Mazingira salama (HSSE). Tunapokaribia maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani duniani, kampeni hii inaonyesha azma yetu ya kulinda maisha katika jamii tunazozihudumia,” alisema Mhandisi Hiliyai.

Katika vifo 31 kwa kila watu 100,000, WHO inaripoti kwamba vifo vinavyotokana na ajali za barabarani nchini Tanzania ni karibu mara 1.7 ya kiwango cha kimataifa na juu zaidi ya wastani wa Afrika. Takwimu za Jeshi la Polisi Tanzania zinaonyesha kuwa mwaka 2024 pekee, nchi ilirekodi ajali 1,735 za barabarani ambapo ajali 1,198 kati ya hizo zilisababisha vifo vya Watu 1,715. Makosa ya kibinadamu, ikiwemo kupuuzia alama za barabarani, kuendesha gari kwa uzembe, na mwendokasi, vilichangia 97% ya matukio haya.

Programu ya ‘Be Road Safe Africa’ ni sehemu ya dhamira ya Puma Energy Tanzania ya kusaidia usalama na ustawi wa jamii, hasa jamii zilizo katika mazingira magumu na maeneo hatarishi. Kupitia mafunzo ya mbinu mbalimbali, mashindano, na uboreshaji wa miundombinu, programu hii inasaidia kuzifanya barabara zetu kuwa salama kwa watoto wa shule nchini.

Afisa mnadhimu wa Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP) Butusyo Mwambelo, akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ufukoni, Jackson Masamaki, cheti na fedha Sh. 500,000 baada kuibuka mshindi katika mashindano ya kuchora picha zenye ujumbe wa usalama barabarani, zilizotolewa na Puma Energy Tanzania kupitia Kampeni ya Usalama Barabarani mashuleni, katika shule hiyo, Kigamboni, Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa kampuni hiyo, Mhandisi Lameck Hiliyai.

Afisa mnadhimu wa Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP) Butusyo Mwambelo, akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ufukoni, Edger Muyonga, mfano wa hundi ya Sh. milioni tano, baada shule hiyo kuibuka mshindi katika mashindano ya kuchora picha zenye ujumbe wa usalama barabarani, zilizotolewa na Puma Energy Tanzania kupitia Kampeni ya Usalama Barabarani mashuleni, katika shule hiyo, Kigamboni, Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa kampuni hiyo, Mhandisi Lameck Hiliyai.

Afisa mnadhimu wa Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP) Butusyo Mwambelo, akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ufukoni, Edger Muyonga, kombe baada shule hiyo kuibuka mshindi katika mashindano ya kuchora picha zenye ujumbe wa usalama barabarani, zilizotolewa na Puma Energy Tanzania kupitia Kampeni ya Usalama Barabarani mashuleni, katika shule hiyo, Kigamboni, Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa kampuni hiyo, Mhandisi Lameck Hiliyai.

Related Posts