Sababu wahitaji wa viungo kukosa huduma vifaa bandia, mkakati watajwa kuwafikia

Mbeya. Licha ya  Hosptali  ya Rufaa Kanda ya Mbeya kuwekeza ubora wa  huduma ya viungo bandia na vifaatiba saidizi, bado kuna changamoto  ya baadhi wagonjwa  kushindwa kuzifikia  kutokana na hali duni ya uchumi na ukosefu elimu hususani  maeneo ya vijijijni.

Imeelezwa  kuwa idara ya viungo bandia kwa mwaka ufikiwa na kutoa huduma kwa  wastani  wa zaidi ya wagonjwa zaidi ya 800   huku asilimia 40 mpaka 50 wakiwepo wanaume na watoto  hunufaika .

Miongoni  mwa mikakati ni kutoa elimu  kupitia mitandao ya kijamii ya hospitali kufikisha taarifa za uwepo wa huduma za  viungo bandia lengo ni kuona jamii yenye uhitaji inarejesha tabasamu.

Ofisa Mteknolojia  Viungo Bandia na Mkuu ya  Kitengo hicho,  Beatrice Hankungwe amesema leo Jumanne Julai 2,2025 wakati akizungumza  na Mwananchi  Digital kuhusiana na hali ya utoaji huduma na mwamko wa wagonjwa kuzifikia hususani waliopata ajali za barabarani ili kurejesha tabasamu.

“Unajua huduma hizo zinalipiwa, lakini kuna wakati  kuna wadau  wanafika kusapoti nasi tunawatangazia wananchi mikoa ya Kanda yetu  wanafika kuwekewa viungo bandia bure  na kurejesha tabasamu wakiwepo  watoto wadogo wanaobainika na changamoto  za kuzaliwa,” amesema.

Ametaja miongoni na visababisha vya wagonjwa wanaofika kupatiwa huduma ya viungo  bandia na vifaa tiba saidizi ni pamoja na wanaopatwa  ajali saratani, kisukari, huku kundi kubwa ni wanaume.

Kwa upande watoto ametaja visababishi kuwa ni udhaifu wa mwili tangu wanapozaliwa  hususani changamoto  ya mtindio wa ubongo,mgongo wazi ,vichwa vikubwa na mengine yanayo husiana  na hayo.

“Kimsingi kati ya asilimia 40 mpaka 50 ya wagonjwa  tunao wahudumia wanaume ni wengi kuliko makundi mengine ,lakini tunatambua  ni sehemu ya kundi ambalo ufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ambazo uweza kusababisha ajali,” amesema.

Amesema wanaomba wadau kujitokeza kusaidia kulipia gharama kwa  wenye mahitaji waweze kurejesha tabasamu  kama jamii nyingine.

Katika hatua nyingine Beatrice,  amesema elimu zaidi yahitajika kwa jamii kufuatia Serikali ya awamu ya sita kuwekeza katika  kuboresha huduma za afya kwenye Hosptali  ya Kanda  ni wakati sasa kutumia fursa hiyo ili kurejesha tabasamu kwa ndugu na jamaa yenye mahitaji ya viungo bandia hususani miguu, mikono na matiti kwa wanawake.

Kwa upande wake, Ofisa mteknolojia viungo tiba na vifaa tiba saidizi  Hosptali ya Kanda, Hemed Shalua amesema kutokana na elimu ndogo kwa jamii kuzifikia huduma wameweke mikakati mbalimbali  ya kuwafikia hususani maeneo ya vijijini.

“Unajua furaha ya mwanadamu ni kuwa na uwezo wa kutekeleza  majukumu  ya utafutaji akiwa salama hivyo tunawasihi wenye changamoto kufika sambamba na kuomba Serikali  kuongeza wataalamu kwenye idara hiyo kulingana na mahitaji,” amesema.

Sikitu Anthon Mkazi wa Iyunga jijini hapa,amesema  ili wenye uhitaji  kukimbilia huduma hizo ni vyema Serikali  ingaanjia njia mbadala ya kusaidia kundi ambalo ukata umekuwa changamoto.

“Wapo watu mitaani anatambalia chini baada ya kupata ulemavu wa kudumu ambao hutokana na ajali,  lakini kutokana  na gharama za tiba  analazika kuishi kwa matumizi  kwa kukata tamaa ya maisha,” amesema.