Klabu ya Simba SC imeendelea kuimarisha kikosi chake kwa msimu ujao kwa kumsajili kiungo mshambuliaji kutoka Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars), Mohamed Bajaber.
Bajaber (miaka 22), ambaye alikuwa akikipiga Kenya Police FC, amesaini mkataba wa miaka miwili ambao utamuweka Msimbazi hadi Juni 2027.
Ni sehemu ya mikakati ya Wekundu wa Msimbazi kujenga kikosi imara kuelekea msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa.