INEC KUSHIRIKIANA KWA KARIBU NA VYOMBO VYA HABARI KATIKA UCHAGUZI MKUU 2025

 

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima akizungumza katika Mkutano wa Tume, Wahariri na Waandishi wa Habari, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2025 ambapo amewakikishia washiriki hao kuwa, ofisi yake itafanya kazi kwa karibu katika kipindi cha uchaguzi mkuu kwa njia mbalimbali ikiwemo kushiriki katika vipindi vya redio na runinga na kutoa taarifa kwa wakati.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima akizungumza katika Mkutano wa Tume, Wahariri na Waandishi wa Habari, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2025 ambapo amewakikishia washiriki hao kuwa, ofisi yake itafanya kazi kwa karibu katika kipindi cha uchaguzi mkuu kwa njia mbalimbali ikiwemo kushiriki katika vipindi vya redio na runinga na kutoa taarifa kwa wakati.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Giveness Aswile akizungumza katika Mkutano wa Tume, Wahariri na Waandishi wa Habari, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2025.

***************

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeahidi kutoa ushirikiano wa karibu kwa vyombo vya habari nchini katika kuhakikisha taarifa za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 zinapatikana kwa wakati na kwa usahihi.

Akifungua mafunzo ya Wahariri na Waandishi wa Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 katika ukumbi wa Mlimani City leo tarehe 4 Agosti 2025, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndugu Kailima R.K., amesema katika kipindi hiki cha uchaguzi, Tume itashirikiana na waandishi wa habari kupitia njia mbalimbali ikiwemo kushiriki katika vipindi vya redio na televisheni, pamoja na kutoa taarifa rasmi kwa wakati unaofaa ili kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa habari za kweli na zisizo na upotoshaji.

“Tunaamini kuwa vyombo vya habari vina nafasi muhimu katika kuhakikisha mchakato wa uchaguzi unafanyika kwa amani. Kwa hiyo, tutaendelea kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha habari zinazotolewa zinazingatia maadili ya uandishi wa habari na kuepuka maudhui yanayoweza kuchochea chuki au ghasia,” amesema Ndugu Kailima.

Mkurugenzi wa Uchaguzi amesisitiza kuwa Tume itatoa taarifa sahihi na kwa wakati, na itatoa ushirikiano kwa waandishi wa habari kila wanapohitaji ufafanuzi au msaada wowote wa kihabari.

Aidha, Ndugu Kailima ameeleza kuwa Tume itazindua mfumo wa kusajili vyombo vya habari kuanzia tarehe 1 hadi 30 Septemba 2025.

“Mfumo huu utasaidia vyombo vya habari kupata vibali na vitambulisho rasmi vya waandishi wake kwa ajili ya kufanikisha kazi zao wakati wa Uchaguzi Mkuu,” ameeleza.

Kufanyika kwa mafunzo kwa Wahariri na Waandishi wa Habari kumehitimisha mfululizo wa mikutano ya wadau ambayo ilianza tangu tarehe 27 Julai 2025, ambapo Tume ilikutana na viongozi wa vyama vya siasa, asasi zisizo za kiserikali, 

wawakilishi wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, wahariri wa vyombo vya habari, waandishi wa habari na watayarishaji wa maudhui ya mtandaoni.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima akizungumza katika Mkutano wa Tume, Wahariri na Waandishi wa Habari, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2025 ambapo amewahakikishia washiriki hao kuwa, ofisi yake itafanya kazi nao kwa karibu katika kipindi cha uchaguzi mkuu kwa njia mbalimbali ikiwemo kushiriki katika vipindi vya redio na runinga na kutoa taarifa kwa wakati.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima (Katikati waliokaa), Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Giveness Aswile (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Daftari na TEHAMA, Stanslaus Mwita (kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria Selemani Mtibora (wa pili kulia), na Mwenyekiti wa Mafunzo ya Wahariri na Waandishi wa Habari, Lilian Timbuka (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahariri na waandishi wa habari baada ya kufunguliwa kwa mafunzo hayo katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, leo Agosti 4, 2025.