Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, ametoa msimamo wake wazi juu ya kiungo mshambuliaji, Ladack Chasambi, akibainisha kuwa hayupo katika mipango yake ya msimu ujao.
Inaelezwa kuwa Fadlu hana mpango wa Chasambi katika nafasi ya winga, na hivyo amempa chaguo muhimu: kama Chasambi anataka kubaki klabuni, basi lazima ajitahidi kubadilika na kuonyesha uwezo katika nafasi ya beki wa kulia.
Chanzo chetu kilieleza kuwa, kocha Davids pia amefungua mlango wa kuondoka kwa kiungo huyo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho, ikiwa akipata ofa nzuri kwingine.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.