-DKT. BITEKO AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO VIKAO VYA KIMKAKATI VYA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akimkabidhi Cheti Mwenyekiti wa Bodi ya Hifadhi ya Ngorongoro, Jenerali Venance Mabeyo wakati wa ufungaji wa Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs Forum 2025) kilichofanyika Agosti 26, 2025 katika Ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Cheti hicho kimekabidhiwa kwa kuwa NCAA imekuwa sehemu ya wadhamini wa kikao hicho.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akifunga Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs Forum 2025) kilichofanyika jijini Arusha katika Ukumbi wa AICC

……………………….

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewahimiza Wenyeviti na Wakuu wa  Taasisi za
Umma nchini kusimamia
utekelezaji wa
maazimio ya kimkakati yanayofikiwa katika vikao kazi
wanavyofanya kwa kutambua kuwa wamebeba dhamana ya
kuboresha maisha ya
Watanzania kupitia
mtaji wa shilingi Trilioni 86 ambao Serikali
imewekeza kwenye Taasisi na mashirika yake..

Dkt. Biteko ameyasema hayo tarehe 26 Agosti 2025
jijini Arusha wakati

akifunga kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na
Watendaji Wakuu wa

Taasisi za Umma (CEOs FORUM 2025).

 “Watanzania wanawategemea ninyi kuwabadilishia maisha, kama tunazungumza kuhusu
umaskini wa watu,
Serikali inapaswa kuwa
kiongozi wa kuwaondolea watu umaskini wao,
hivyo
hamna budi kutambua  kuwa mnalo deni la
kuboresha hali zetu na maisha yetu.” Amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko amewahakikishia Watendaji hao kuwa
Serikali katika ngazi

zote inatambua mchango wa taasisi na mashirika katika ukuaji wa uchumi na pia inatambua
mchango wa vikao
kazi vya watendaji hao
ambavyo vimepelekea mashirika kuongeza mchango
wake katika mfuko mkuu wa Taifa.

” Vikao kazi hivi mnavyofanya vimeonesha
mchango wake katika uchumi,

mfano katika kikao kazi cha mwaka 2024 mliazimia
mashirika ya umma

yaboreshe utendaji na  kuongeza uchangiaji
katika mfuko mkuu wa
Serikali na 
matokeo yameonekana mfano Shirika la Maendeleo ya Petroli
( TPDC) liliongeza uchangiaji wake kwa asilimia 100,
shirika hili
liliongeza uchangiaji wake
kutoka shilingi bilioni 5.5 kwa mwaka
2023/2024
hadi shilingi bilioni 11.1 mwaka 2024/2025.” Amesema
Dkt.Biteko

Ameongeza kuwa, uchagiaji wa Shirika la Nyumba
la Taifa (NHC)
umeongezeka kwa 
asilimia 363 katika mfuko mkuu wa Serikali ambapo NHC
ilichangia shilingi bilioni 1.2 mwaka 2023/ 24 na
mwaka 2024/2025
ilichangia shilingi
bilioni 5.5.

Dkt. Biteko amewaeleza Wenyeviti wa Bodi na
Wakuu wa Taasisi kuwa
“Rais Samia pamoja
na kuthamini mchango wenu kwa Serikali anatarajia
mengi kutoka kwenu na Watanzania wana matarajio
makubwa hasa wakati
tukielekea
kwenye  utekelezaji wa Dira 2050, endeleeni  kuongeza
mchango wenu kwenye  ukuaji wa uchumi, mjitegemee
na muwe mfano wa
taasisi binafsi.”

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ametaka
viongozi hao kufanyia kazi

agizo lililotolewa na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt.
Philip Isdor Mpango la

 kudhibiti mianya ya uvujaji wa mapato.

Pia amempongeza Msajili wa Hazina kwa kuwa na
maono ya kuratibu kikao

kazi hicho ili kujadili masuala yatakayosukuma
mbele utendaji wa
taasisi.

Katika hafla hiyo, Dkt. Biteko hakuacha
kukumbusha kuhusu ushiriki wa

Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo amesema uchaguzi huo uwe ni ajenda ya watu wote
wakiwemo Wenyeviti  wa
Bodi na Wakuu
wa Taasisi hivyo waone kuwa wana wajibu wa kuwasisitiza
watu kwenye taasisi zao kujitokeza kusikiliza wagombea
na baadaye
kupiga kura  kwa amani
kwani kukiwa na amani mashirika hayo pia
yatafanya
vizuri zaidi.

 Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe.
Stanslaus Nyongo kwa
upande wake,
amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan   kwa dira na
muongozo katika kuendeleza mashirika ya umma ili
yaweze kuwa na tija
nchini.

Amesema katika siku tatu za kikao kazi washiriki
wamejifunza na
kubadilishana uzoefu
kupitia watoa mada wa ndani na nje ya nchi
waliobobea.

Amesema Wizara ya Mipango na Uwekezaji
itahakikisha maazimio ya  kikao
kazi
hicho yanatekelezwa ipasavyo, pia Wizara itasimamia mageuzi ya
kuhakikisha mashirika  ya umma yanachangia ukuaji
wa pato la taifa
hadi kufikia Dola 
za Marekani trilioni 1  ifikapo 2050 ambapo  kwa
sasa pato la taifa ni dola za Marekani bilioni 85.

Kwa upande wake Salim Kali, Kaimu Mkuu wa Mkoa
wa Arusha amesema
wilaya 6 za Mkoa wa
Arusha zimefikiwa na umeme hadi ngazi ya vijiji,
pia  miradi ya maji imefanyika pamoja na  miundombinu ya
Barabara
ambayo imewezesha maisha bora
kwa watu wa aina zote wakiwemo watalii.

Awali, Msajili wa Hazina,  Nehemia Mchechu
alisema kuwa katika kikao
kazi hicho
kampuni zaidi 300 zimeshiriki huku washiriki wakiwa ni
zaidi ya 650.

Alisema kikao kilikuwa na  majadiliano
mbalimbali ya kina yanayolenga
kusukuma
mbele uchumi wa nchi na kusimamia uwekezaji wa Serikali  kwa

taasisi za umma wa zaidi ya shilingi trilioni
86.

Mkutano huo wa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji
Wakuu wa Taasisi za Umma

uliongozwa na kaulimbiu ya 
“Ushirikiano Endelevu wa  Kibiashara

katika Mazingira Shindani Kimataifa- Nafasi ya
Mashirika ya Umma.”

Teresia Xavier Mhagama