Mgombea Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Mariam Ibrahim, leo Septemba 16 ameungana na Umoja wa Wanawake wa Mkoa wa Pwani kufagia viwanja vya Shule ya Msingi Majengo vilivyopo Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.
Hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bagamoyo, Subira Khamis Mgalu, unaotarajiwa kufanyika kesho katika viwanja hivyo.


Aidha, baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo walionesha furaha na kuahidi kujitokeza kesho kwa wingi.
“Tumehamasika sana kuona viongozi wetu wakishiriki kwa vitendo. Hii inatupa moyo wa kushiriki na kuunga mkono kampeni zinazokuja,” alisema Mwanaid Juma, mkazi wa Bagamoyo.