Bado watatu – 53


BAADA ya wiki tatu, Faustin alipelekwa tena mahakamani na mimi nikaendelea na ushahidi wangu ambapo niliieleza mahakama kwamba mshitakiwa amechunguzwa akili yake na amethibitishwa kuwa hakuwa na matatizo ya akili. Nikakitoa cheti cha daktari kilichothibitisha kwamba Faustin alikuwa mzima.