Waziri Kombo akutana na Balozi wa Zambia nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Zambia nchini, Mhe. Mathews Jere kuhusu masuala ya mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa uwili baina ya Tanzania na Zambia.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Kombo ametumia fursa hiyo kutuma salamu za shukrani kwa Rais wa Zambia, Mhe. Hakainde Hichilema kwa ushiriki wake katika hafla ya kumwapisha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa hotuba nzuri iliyogusa mioyo ya wengi waliofanikiwa kuisikia.