DKT. MWIGULU KUMUWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA KWENYE HAFLA YA UTOAJI TUZO ZA UHIFADHI NA UTALII

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 31, 2026 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya Utoaji wa Tuzo za kitaifa za Uhifadhi na Utalii (The Serengeti Awards).

Pia, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu atatembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia katika kukuza Utalii nchini.